< 1 Timotheo 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
Paul, the apostle of Jesus according to the commandment of God our Saviour, and Jesus Christ our hope;
2 Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my beloved son in the faith. Grace, mercy, peace, from God the Father and Jesus Christ our Lord.
3 Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo
As I exhorted you to remain in Ephesus, I going into Macedonia, in order that you may command certain ones not to teach heterodoxy,
4 wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.
nor to give heed to fables and endless genealogies, which present questions, rather than the economy of God which is in faith:
5 Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.
but the end of the commandment is divine love out of a clean heart and a good conscience and faith free from hypocrisy:
6 Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,
from which certain ones having deflected have gone out into empty talking,
7 wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.
wishing to be teachers of the law, not knowing either what they are saying, or concerning what things they do affirm.
8 Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.
But we know that the law is good, if any one may use it lawfully;
9 Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,
knowing this, that the law is not made for the righteous, but for the unrighteous and disorderly, for the ungodly and for sinners, for the unholy and the profane, for patricides, matricides and homocides,
10 kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli,
for fornicators, for Sodomites, for kidnapers, for liars, for perjurers, and if any thing else is opposed to healthy teaching;
11 ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.
according to the gospel of the glory of the blessed God, with which I am intrusted.
12 Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake.
I give thanks to Jesus Christ our Lord, the one having filled me up with dynamite, because he considered me faithful, having put me in the ministry;
13 Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu.
being antecedently a blasphemer, and a persecutor, and an insulter: but I obtained mercy, because I did it in unbelief being ignorant;
14 Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
but the grace of our Lord with faith and the divine love which is in Christ Jesus superabounded.
15 Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote.
It is a faithful saying, and worthy of all acceptation, that Christ Jesus came into the world to save sinners; of whom I am chief:
16 Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
but on this account I obtained mercy, in order that Jesus Christ might in me the chief show forth all longsuffering, for an example of those about to believe on him unto eternal life. (aiōnios g166)
17 Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
But to the King of the ages, the incorruptible, invisible, only God, be honor and glory unto the ages of the ages. Amen. (aiōn g165)
18 Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri,
This charge I commit unto you, O child Timothy, according to the prophecies that went before on you, that you may war a beautiful warfare in the same;
19 ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao.
having faith and a good conscience; which some having cast away have made shipwreck concerning the faith;
20 Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.
of whom is Hymenaeus and Alexander, whom I have delivered to Satan, that they may learn not to blaspheme.

< 1 Timotheo 1 >