< 2 Wakorintho 1 >
1 Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
Pavel, po Božji volji apostol Jezusa Kristusa, in naš brat Timótej Božji cerkvi, ki je v Korintu, z vsemi svetimi, ki so po vsej Ahaji:
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa.‹
3 Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
Blagoslovljen bodi Bog, celó Oče našega Gospoda Jezusa Kristusa, Oče usmiljenj in Bog vse tolažbe,
4 Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
ki nas tolaži v vsaki naši stiski, da bomo sposobni tolažiti te, ki so v kakršnikoli težavi, s tolažbo, s katero smo mi sami potolaženi od Boga.
5 Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
Kajti kakor so Kristusova trpljenja obilna v nas, tako je obilna tudi naša tolažba po Kristusu.
6 Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
Če pa smo stiskani, je to za vašo tolažbo in rešitev duš, ki je učinkovita v prestajanju istih trpljenj, ki jih tudi mi prenašamo; ali če smo potolaženi, je to zaradi vaše tolažbe in rešitve duš.
7 Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
In naše upanje o vas je neomajno, vedoč, da kakor ste udeleženci trpljenj, tako boste postali tudi tolažbe.
8 Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
Kajti nočemo, bratje, da bi bili vi nevedni o naši težavi, ki je k nam prišla v Aziji, da smo bili stiskani preko mere, nad močjo, tako zelo, da smo obupali celó nad življenjem.
9 Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
Toda v sebi smo imeli smrtno obsodbo, da ne bi zaupali vase, temveč v Boga, ki obuja mrtve;
10 Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
ki nas je osvobodil iz tako velike smrti in še osvobaja; v katerega zaupamo, da nas bo še osvobajal.
11 Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
Tudi vi skupaj pomagate z molitvijo za nas, da bi bila lahko zaradi daru, podarjenega nam, s pomočjo mnogih oseb, dana zahvala z naše strani.
12 Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
Kajti naše veselje je to, pričevanje naše vesti, da smo se v svetu vedli s preprostostjo in pobožno iskrenostjo, ne z meseno modrostjo, temveč z Božjo milostjo in bolj obilno posebej do vas.
13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
Kajti ne pišemo vam nobenih drugih stvari, kakor kar berete ali spoznavate; in zaupam, da boste spoznali celó do konca;
14 kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
kakor ste nas tudi vi deloma spoznali, da smo mi vaše veselje, celó kakor ste tudi vi naše na dan Gospoda Jezusa.
15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
V tem zaupanju sem bil voljan prej priti k vam, da bi vi lahko imeli dvojno korist;
16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
in mimo vas iti v Makedonijo in iz Makedonije ponovno priti k vam in bi bil od vas pospremljen na svoji poti proti Judeji.
17 Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
Ko sem bil torej takih misli, ali sem uporabil lahkomiselnost? Ali stvari, ki jih nameravam, nameravam storiti glede na meso, da bo z menoj »da, « »da« in »ne, « »ne«?
18 Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
Toda kakor je Bog resničen, naša beseda do vas ni bila »da« in »ne.«
19 Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
Kajti Božji Sin, Jezus Kristus, ki je bil med vami oznanjen po nas, celó po meni in Silvánu ter Timóteju, ni bil »da« in »ne, « temveč je bil v njem »da.«
20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
Kajti vse Božje obljube so v njem »da« in v njem »Amen« v Božjo slavo po nas.
21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
Torej tisti, ki nas z vami utrjuje v Kristusu in nas je mazilil, je Bog;
22 kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
ki nas je tudi zapečatil in v naša srca dal poroštvo Duha.
23 Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
Poleg tega kličem Boga za pričo nad svojo dušo, da doslej še nisem prišel k vam v Korint, da bi vam prizanesel.
24 Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.
Ne, ker bi imeli gospostvo nad vašo vero, temveč smo pomočniki vaše radosti; kajti stojite po veri.