< 1 Wakorintho 1 >
1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
Pavel, poklican, da je po Božji volji apostol Jezusa Kristusa in naš brat Sostén,
2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
Božji cerkvi, ki je v Korintu, tem, ki so posvečeni v Kristusu Jezusu, poklicani, da so sveti, z vsemi, ki na vsakem kraju, tako njihovem kakor našem, kličejo ime Jezusa Kristusa, našega Gospoda:
3 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa.‹
4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
Vedno se vam v prid zahvaljujem svojemu Bogu za Božjo milost, ki vam je dana po Jezusu Kristusu,
5 Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
da ste v vsaki stvari obogateni po njem, v vsej izgovarjavi in v vsem spoznanju;
6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
celó kakor je bilo Kristusovo pričevanje potrjeno v vas,
7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
tako da vam, ki pričakujete prihod našega Gospoda Jezusa Kristusa, ne primanjkuje nobenega daru;
8 Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
ki vas bo tudi do konca potrdil, da boste lahko brez krivde na dan našega Gospoda Jezusa Kristusa.
9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
Bog je zvest, po katerem ste bili poklicani v družbo njegovega Sina Jezusa Kristusa, našega Gospoda.
10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
Torej vas rotim, bratje, v imenu našega Gospoda Jezusa Kristusa, da vsi govorite isto stvar in da med vami ne bo nobenih nesoglasij; temveč da boste popolnoma združeni skupaj, v istem mišljenju in v isti sodbi.
11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
Kajti razodeto mi je bilo o vas, moji bratje, po teh, ki so iz Hloine hiše, da so med vami prepiri.
12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
Pravim torej to, da vsak izmed vas govori: »Jaz sem Pavlov, jaz Apolov, jaz Kefov, jaz pa Kristusov.«
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Ali je Kristus razdeljen? Ali je bil Pavel križan za vas? Ali ste bili krščeni v Pavlovo ime?
14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
Zahvaljujem se Bogu, da nisem krstil nobenega izmed vas razen Krispa in Gaja,
15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
da ne bi kdorkoli lahko rekel, da sem krščeval v svojem lastnem imenu.
16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
In krstil sem tudi Stefanájevo družino; razen tega ne vem, če sem krstil kogarkoli drugega.
17 Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
Kajti Kristus me ni poslal krščevat, temveč oznanjat evangelij; ne z modrostjo besed, da ne bi bil Kristusov križ storjen brez učinka.
18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
Kajti oznanjevanje križa je tem, ki propadajo, nespametnost; toda nam, ki smo rešeni, je Božja moč.
19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
Kajti pisano je: ›Uničil bom modrost modrih in zavrgel bom razum razsodnih.‹
20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn )
Kje je modri? Kje je pisar? Kje je razpravljavec tega sveta? Mar ni modrosti tega sveta Bog naredil za nespametnost? (aiōn )
21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
Kajti potem, ko v Božji modrosti svet po modrosti ni spoznal Boga, je Bogu ugajalo, da po nespametnosti oznanjevanja reši te, ki verujejo.
22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
Kajti Judje zahtevajo znamenje in Grki iščejo modrost,
23 Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
toda mi oznanjamo križanega Kristusa, Judom kamen spotike in Grkom nespametnost;
24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
toda tem, ki so poklicani, tako Judom kakor Grkom, [je] Kristus Božja moč in Božja modrost.
25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
Kajti Božja nespametnost je modrejša od ljudi in Božja slabost močnejša od ljudi.
26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
Kajti vidite svoj klic, bratje, da ni poklicanih veliko modrih po mesu, ne veliko mogočnih, ne veliko plemenitih;
27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
toda Bog je izbral nespametne stvari sveta, da zbega modre; in Bog je izbral slabotne stvari sveta, da zbega stvari, ki so mogočne;
28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
in nizke stvari sveta in stvari, ki so prezirane, je Bog izbral, da, in stvari, ki niso, da zavrže stvari, ki so,
29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
da se v njegovi prisotnosti ne bi poveličevalo nobeno meso.
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
Toda vi ste iz njega v Kristusu Jezusu, ki je za nas postal modrost od Boga in pravičnost in posvečenje in odkupitev;
31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
da, kakor je pisano: ›Kdor se ponaša, naj se ponaša v Gospodu.‹