< 2 Wakorintho 8 >

1 Basi sasa ndugu, nataka ninyi mjue kuhusu ile neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia.
We want you to know, brothers, about the grace of God that has been given to the churches of Macedonia.
2 Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha waliyokuwa nayo ilikuwa kubwa, ingawa walikuwa maskini kupindukia, kwa upande wao walifurika kwa wingi wa ukarimu.
During a great test of affliction, the abundance of their joy and the extremity of their poverty have produced great riches of generosity.
3 Kwa maana nashuhudia kwamba wao walitoa kwa kadiri wawezavyo, hata na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe,
For I bear witness that they gave as much as they were able, and even beyond what they were able, and of their own free will,
4 wakitusihi kwa bidii wapewe fursa ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watakatifu.
they urgently pleaded with us for the privlege of sharing in this ministry to the believers.
5 Wala hawakufanya tulivyotazamia, bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwa ajili yetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
This did not happen as we had expected. Instead, they first gave themselves to the Lord. Then they gave themselves to us by the will of God.
6 Kwa hiyo tulimsihi Tito, kwa kuwa ndiye alianzisha jambo hili, akamilishe tendo hili la neema kwa upande wenu.
So we urged Titus, who had already begun this task, to complete among you this act of grace.
7 Lakini kama vile mlivyo mbele sana katika yote: Katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika uaminifu wote na katika upendo wenu kwetu sisi, vivyo hivyo tunataka pia mzidi katika neema hii ya kutoa.
But you abound in everything—in faith, in speech, in knowledge, in all diligence, and in your love for us. So also make sure that you excel in this act of grace.
8 Siwaamrishi, lakini nataka kujaribu unyofu wa upendo wenu kwa kuulinganisha na bidii ya wengine.
I say this not as a command. Instead, I say this in order to test the sincerity of your love by comparing it to the eagerness of other people.
9 Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri.
For you know the grace of our Lord Jesus Christ. Even though he was rich, for your sakes he became poor, so that through his poverty you might become rich.
10 Ushauri wangu kuhusu lile lililo bora kwenu juu ya jambo hili ni huu: Mwaka uliopita ninyi mlikuwa wa kwanza si tu kutoa lakini pia mlikuwa na shauku ya kufanya hivyo.
In this matter I will give you advice that will help you. One year ago, you not only started to do something, but you desired to do it.
11 Sasa ikamilisheni kazi hii kwa shauku kama mlivyoanza, jitoleeni kulingana na uwezo wenu.
Now finish it. Just as there was an eagerness and desire to do it then, may you also bring it to completion, as much as you can.
12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kulingana na kile mtu alicho nacho, wala si kwa kile ambacho hana.
For if you are eager to do this deed, it is a good and acceptable thing. It must be based on what a person has, not on what he does not have.
13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka, bali pawe na uwiano.
For this task is not in order that others may be relieved and you may be burdened. Instead, there should be fairness.
14 Kwa wakati huu, wingi wa vitu mlivyo navyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao watakapokuwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu.
Your abundance at the present time will supply what they need. This is also so that their abundance may supply your need, and so that there may be fairness.
15 Ndipo patakuwa na usawa, kama ilivyoandikwa: “Aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
It is as it is written: “The one with much did not have anything left over, and the one who had little did not have any lack.”
16 Ninamshukuru Mungu ambaye amemtia Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali.
But thanks be to God, who put into Titus' heart the same earnest care that I have for you.
17 Si kwamba Tito amekubali tu ombi letu, bali anakuja kwenu akiwa na shauku kuliko wakati mwingine, tena kwa hiari yake mwenyewe.
For he not only accepted our appeal, but he was also very earnest about it. He came to you of his own free will.
18 Nasi tunamtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili.
We have sent with him the brother who is praised among all of the churches for his work in proclaiming the gospel.
19 Zaidi ya hayo, alichaguliwa na makanisa ili asafiri pamoja nasi tulipokuwa tunapeleka matoleo ya ukarimu, kwa ajili ya utukufu wa Bwana mwenyewe, na ili kuonyesha hisani yetu kuwasaidia.
Not only this, but he also was selected by the churches to travel with us in our carrying out this act of grace. This is for the honor of the Lord himself and for our eagerness to help.
20 Tunataka kuepuka lawama yoyote kuhusu jinsi tunavyosimamia matoleo haya ya ukarimu.
We are avoiding the possibility that anyone should complain about us concerning this generosity that we are carrying out.
21 Kwa kuwa tunakusudia kufanya kile kilicho haki si machoni mwa Bwana peke yake, bali pia machoni mwa watu wengine.
We take care to do what is honorable, not only before the Lord, but also before people.
22 Pamoja nao, tunamtuma ndugu yetu ambaye mara kwa mara ametuthibitishia kwa njia nyingi kwamba ana shauku, naam, zaidi sana sasa kwa sababu analo tumaini kuu kwenu.
We are also sending another brother with them. We have tested him in many ways and found him diligent for many tasks. He is even more eager now because of the great confidence he has in you.
23 Kwa habari ya Tito, yeye ni mwenzangu na mtendakazi pamoja nami miongoni mwenu. Kwa habari za ndugu zetu, wao ni wawakilishi wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
As for Titus, he is my partner and fellow worker for you. As for our brothers, they are sent by the churches. They are an honor to Christ.
24 Kwa hiyo waonyesheni wazi hawa ndugu uthibitisho wa upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, mbele ya makanisa, ili yapate kuona.
So show them your love, and show to the churches the reason for our boasting about you.

< 2 Wakorintho 8 >