< 2 Wakorintho 10 >
1 Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi!
But I Paul exhort you through the meekness and gentleness of Christ, who before your face am indeed humble among you, but being absent am bold towards you:
2 Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu.
but I pray, that being present I may not be bold with the confidence with which I consider myself bold towards certain ones who regard us as walking about according to the flesh.
3 Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo.
For walking in the flesh, we do not wage war according to the flesh;
4 Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,
for the weapons of our warfare are not carnal, but mighty to God unto the pulling down of strongholds;
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo,
casting down imaginations, and every high thing that exalts itself against the knowledge of God, and bringing into captivity every thought to the obedience of Christ;
6 tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.
and being ready to avenge every disobedience, when your obedience may be complete.
7 Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
Do you look at things according to the outward appearance? If any has trusted to himself that he belongs to Christ, let him again consider this in reference to himself, that as he belongs to Christ, so do we also.
8 Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya.
For if I shall in any thing the more abundantly boast concerning our power which the Lord gave us for your edification, and not for your destruction, I will not be ashamed:
9 Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu.
in order that I may not seem as it were to terrify you by my letters.
10 Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.”
Because they say, His letters are indeed weighty and powerful; but the presence of his body is weak, and his speech contemptible.
11 Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.
Let such a one consider this, that, such as we are in word by our letters while absent, such we really are in work being present.
12 Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara.
For we are not bold to number or compare ourselves with certain ones of those who recommend themselves: but they, measuring themselves by themselves, and comparing themselves to themselves, are not wise.
13 Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi.
But we will not boast in things without measure, but according to the measure of the rule which measure God has measured to us, to reach even unto you.
14 Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo.
For not as not reaching unto you do we stretch ourselves, for we have advanced in the gospel of Christ even unto you:
15 Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
and not boasting in things without measure, in the labors of others, but having hope of your faith increasing among you, to be magnified according to our rule exceedingly,
16 ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
to preach the gospel in the regions beyond you, not to glory according to the rule of others in things made ready.
17 Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
But he that glorieth, let him glory in the Lord;
18 Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.
for he that commends himself is not approved, but whom the Lord commends.