< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an apostle, not from men, nor through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead,
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren who are with me, to the churches of Galatia.
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Grace to you and peace from God the Father, and our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave Himself for our sins, in order that he might redeem us from the present evil age, according to the will of God even our Father: (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
To whom be glory unto the ages of the ages. Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I am astonished that you are so quickly removed from him who called you in the grace of Christ into another gospel;
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
which is not another: but there are certain ones who are troubling you, and wishing to pervert the gospel of Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But indeed if we, or an angel from heaven, may preach unto you any other gospel except that which we have preached unto you, let him be accursed.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have before said, and now again I tell you, If any one preaches to you a gospel except that which you have received, let him be accursed.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For must I now believe men, or God? whether do I seek to please men? if I were still pleasing men, I would not be the servant of Christ.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
But I make known to you, brethren, the gospel was preached to me, that it is not according to a man;
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
for I did not receive it from man, neither was I taught it, but through the revelation of Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For you have heard of my life formerly in Judaism, that I was persecuting the church of God exceedingly, and destroying it:
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and I was prominent in Judaism above many comrades in my race, being exceedingly zealous of the traditions of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
When the one having separated me, from the womb of my mother, and called me through his grace, was pleased
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
to reveal his Son in me, that I might preach him among the Gentiles; immediately I conferred not with flesh and blood:
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
neither did I go up to Jerusalem to those who were apostles before me; but I went away into Arabia, and returned again to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then after three years I went up to Jerusalem to see Cephas, and remained with him fifteen days;
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
but I saw no other of the apostles, except James the brother of the Lord.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Which things moreover I write unto you, behold, before God, that I lie not.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Then I went into the regions of Syria and Cilicia.
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
But I was unknown by face to the churches of Judea which are in Christ.
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
But they were only hearing that The one persecuting us at one time is now preaching the faith which he was once desolating;
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
and they continued to glorify God in me.

< Wagalatia 1 >