< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Forsothe whanne twenti yeer weren fillid, aftir that Salomon bildide the hows of the Lord,
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
and his owne hows, he bildide the citees, whiche Iram hadde youe to Salomon; and he made the sones of Israel to dwelle there.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Also he yede in to Emath of Suba, and gat it.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
And he bildide Palmyram in deseert, and he bildide othere `citees maad ful stronge in Emath.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
And he bildide the hiyere Betheron and the lowere Betheron, wallid citees, hauynge yatis and lockis and barris;
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
also he bildide Balaath, and alle `citees ful stronge that weren of Salomon; and alle the citees of cartis, and the citees of knyytis kyng Salomon bildide, and disposide alle thingis whiche euere he wolde, in Jerusalem, and in the Liban, and in al the lond of his power.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Salomon made suget in to tributaries til in to this dai al the puple that was left of Etheis, and Amorreis, and Phereseis, and Eueis, and of Jebuseis, that weren not of the generacioun of Israel, and of the sones of hem,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
and of the aftircomers of hem, whiche the sones of Israel hadden not slayn.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Sotheli of the sones of Israel he settide not, that thei schulden serue the werkis of the kyng; for thei weren men werriours, and the firste duykis, and princes of charis, and of hise knyytis;
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
forsothe alle the princes of the oost of kyng Salomon weren two hundrid and fifti, that tauyten the puple.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Sotheli he translatide the douyter of Farao fro the citee of Dauid in to the hows, which he hadde bildid to hir; for the kyng seide, My wijf schal not dwelle in the hows of Dauid, kyng of Israel, for it is halewid, for the arke of the Lord entride in to that hows.
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Thanne Salomon offride brent sacrifices to the Lord on the auter of the Lord, which he hadde bildid bifor the porche,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
that bi alle daies me schulde offre in it, bi the comaundement of Moises, in sabatis, and in kalendis, and in feeste daies, thries bi the yeer, that is, in the solempnyte of the therflooues, and in the solempnyte of woukis, and in the solempnyte of tabernaclis.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
And he ordeynede bi the ordynaunce of Dauid, his fadir, the officis of preestis in her seruyces, and the dekenes in her ordre, that thei schulden preise and mynystre bifor preestis bi the custom of ech dai; and he ordeynede porteris in her departyngis bi yate and yate. For Dauid, the man of God, hadde comaundid so;
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
and bothe preestis and dekenes passiden not fro the comaundementis of the kyng of alle thingis whiche he hadde comaundid.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
And Salomon hadde alle costis maad redi in the kepingis of tresouris, fro that dai in whiche he foundide the hows of the Lord til in to the dai in which he perfourmyde it.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Thanne Salomon yede in to Asiongaber, and in to Hailath, at the brynke of the reed see, which is in the lond of Edom.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
Therfor Iram sente to hym, by the hondis of his seruauntis, schippis, and schippe men kynnyng of the see, and thei yeden with the seruauntis of Salomon in to Ophir, and thei token fro thennus foure hundrid and fifti talentis of gold, and brouyten to kyng Salomon.

< 2 Nyakati 8 >