< 2 Nyakati 7 >

1 Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu wa Bwana ukalijaza Hekalu.
And whanne Salomon schedynge preyeris hadde fillid, fier cam doun fro heuene, and deuouride brent sacrifices, and slayn sacrifices; and the maieste of the Lord fillide the hows.
2 Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu la Bwana kwa sababu utukufu wa Bwana ulilijaza.
And preestis myyten not entre in to the temple of the Lord; for the maieste of the Lord hadde fillid the temple of the Lord.
3 Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu wa Bwana ukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, nao wakamwabudu na kumshukuru Bwana wakisema, “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.”
But also alle the sones of Israel sien fier comynge doun, and the glorie of the Lord on the hows, and thei felden down lowe to the erthe on the pawment araied with stoon, and thei worschipiden, and preisiden the Lord, For he is good, for his merci is in to al the world.
4 Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana Mungu.
Forsothe the kyng and al the puple offriden slayn sacrifices bifor the Lord.
5 Naye Mfalme Solomoni akatoa dhabihu ya ngʼombe 22,000 pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoweka wakfu Hekalu la Mungu.
Therfor king Salomon killide sacrifices of oxis two and twenti thousynd, of wetheris sixe score thousynde; and the kyng and al the puple halewiden the hows of God.
6 Makuhani wakasimama kwenye nafasi zao, vivyo hivyo Walawi wakiwa na vyombo vya uimbaji vya Bwana ambavyo Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza kwa ajili ya kumsifu Bwana, navyo vilitumika wakati aliposhukuru, akisema, “Upendo wake wadumu milele.” Mkabala na Walawi, makuhani walipiga tarumbeta zao, nao Waisraeli wote walikuwa wamesimama.
Forsothe the preestis stoden in her offices, and dekenes in orguns of songis of the Lord, whiche kyng Dauid made to preise the Lord, For his merci is in to the world; and thei sungen the ympnes of Dauid bi her hondis; sotheli the prestis sungen with trumpis bifor hem, and al the puple of Israel stood.
7 Solomoni akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba aliyokuwa ametengeneza haikutosha kuweka sadaka hizo zote za kuteketezwa, sadaka za nafaka na za mafuta.
Therfor Salomon halewide the myddil of the large place bifor the temple of the Lord; for he hadde offrid there brent sacrifices, and the ynnere fatnesses of pesible sacrifices, for the brasun auter which he hadde maad myyte not susteyne the brent sacrifices, and sacrifices, and the innere fatnessis of pesible sacrifices.
8 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu wakati ule kwa muda wa siku saba, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri.
Therfor Salomon made a solempnyte in that tyme in seuene dayes, and al Israel with hym, a ful greete chirche, fro the entryng of Emath `til to the stronde of Egipt.
9 Katika siku ya nane walifanya kusanyiko, kwa kuwa walikuwa wanaadhimisha kuwekwa wakfu kwa madhabahu kwa muda wa siku saba na sikukuu kwa muda wa siku nyingine saba zaidi.
And in the eiythe dai he made a gaderyng of money, `that is, for necessaries of the temple, for he hadde halewid the auter in seuene daies, and `hadde maad solempnytee in seuene daies.
10 Katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa saba Solomoni akawaaga watu waende nyumbani mwao, wakishangilia na kufurahi mioyoni mwao, kwa wema mwingi Bwana Mungu aliomtendea Daudi na Solomoni na kwa ajili ya watu wake Israeli.
Therfor in the thre and twentithe dai of the seuenthe monethe he lete the puplis go to her tabernaclis, ioiynge and gladynge on the good that God hadde do to Dauid, and to Salomon, and to his puple Israel.
11 Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu la Bwana na jumba la kifalme, naye akiwa amefanikiwa kutenda yale yote aliyokuwa nayo moyoni mwake kufanya katika Hekalu la Bwana na katika jumba lake mwenyewe la kifalme,
And Salomon parformyde the hows of the Lord, and the hows of the kyng, and alle thingis which he hadde disposid in his herte for to do in the hows of the Lord and in his owne hows; and he hadde prosperite.
12 Bwana akamtokea Solomoni usiku na kumwambia: “Nimesikia maombi yako nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe kuwa Hekalu kwa ajili ya dhabihu.
Forsothe the Lord aperide to hym in the nyyt, and seide, Y haue herd thi preiere, and Y haue chose this place to me in to an hows of sacrifice.
13 “Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu,
If Y close heuene, and reyn cometh not doun, and if Y sende, and comaunde to a locuste, that he deuoure the lond, and if Y send pestilence in to my puple;
14 kama watu wangu, wanaoitwa kwa Jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao.
forsothe if my puple is conuertid, on whiche my name is clepid, and if it bisechith me, and sekith my face, and doith penaunce of hise werste weies, Y schal here fro heuene, and Y schal be merciful to the synnes of hem, and Y schal heele the lond of hem.
15 Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa.
And myn iyen schulen be openyd, and myn eeren schulen be reisid to the preiere of hym, that preieth in this place;
16 Kwa maana sasa nimechagua na kutakasa Hekalu hili ili kwamba Jina langu lipate kuwa huko milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwepo huko daima.
for Y haue chose, and halewid this place, that my name be there with outen ende, and that myn iyen and myn herte dwelle there in alle daies.
17 “Kwa habari yako wewe, kama ukienenda mbele zangu kama Daudi baba yako alivyoenenda na kufanya yote nikuamuruyo, nawe ukizishika amri zangu na sheria zangu,
Also if thou gost bifore me, as Dauid thi fadir yede, and doist bi alle thingis whiche Y comaundide to thee, and kepist my riytwisnessis and domes, Y schal reise the trone of thi rewme,
18 Nitakiimarisha kiti chako cha enzi kama nilivyoagana na Daudi baba yako niliposema, ‘Hutakosa kamwe mtu wa kutawala juu ya Israeli.’
as Y bihiyte to Dauid thi fadir, and seide, A man of thi generacioun schal not be takun awei, that schal be prince in Israel.
19 “Lakini kama ukigeuka na kuyaacha maagizo na amri nilizowapa na kwenda kuitumikia miungu mingine na kuiabudu,
But if ye turnen awey, and forsake my riytwisnessis and my comaundementis whiche Y settide forth to you, and ye goen, and seruen alien goddis, and worschipen hem,
20 ndipo nitakapoingʼoa Israeli kutoka nchi yangu niliyowapa, nami nitalikataa Hekalu hili nililolitakasa kwa ajili ya Jina langu. Nitalifanya kitu cha kudharauliwa na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa watu wote.
Y schal drawe you awey fro my lond, which Y yaf to you, and Y schal caste awey fro my face this hows which Y haue bildid to my name, and Y schal yyue it in to a parable, and in to ensaumple to alle puplis.
21 Ingawa Hekalu hili linavutia sana sasa, wote watakaolipita watashangaa na kusema, ‘Kwa nini Bwana amefanya kitu kama hiki katika nchi hii na kwa Hekalu hili?’
And this hows schal be in to a prouerbe to alle men passynge forth; and thei schulen seie, wondringe, Whi dide the Lord so to this lond, and to this hows?
22 Watu watajibu, ‘Ni kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa Misri, nao wamekumbatia miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia, ndiyo sababu ameyaleta maafa haya yote juu yao.’”
And thei schulen answere, For thei forsoken the Lord God of her fadris, that ledde hem out of the lond of Egipt, and thei token alien goddis, and worschipiden, and herieden hem; therfor alle these yuelis camen on hem.

< 2 Nyakati 7 >