< 2 Nyakati 27 >

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Yotam yirmi beş yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de on altı yıl krallık yaptı. Annesi Sadok'un kızı Yeruşa'ydı.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
Babası Uzziya gibi, Yotam da RAB'bin gözünde doğru olanı yaptı. Ancak RAB'bin Tapınağı'na girmedi. Ne var ki, halk kötülük yapmayı sürdürmekteydi.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
Yotam RAB'bin Tapınağı'nın Yukarı Kapısı'nı onardı. Ofel Tepesi'ndeki surun üzerinde de birçok iş yaptı.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
Yahuda'nın dağlık bölgesinde kentler, ormanlık tepelerinde kaleler ve kuleler kurdu.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
Ammon Kralı'yla savaşarak Ammonlular'ı yendi. Ammonlular o yıl için kendisine yüz talant gümüş, on bin kor buğday, on bin kor arpa verdiler. İkinci ve üçüncü yıllar için de aynı miktarı ödediler.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
Tanrısı RAB'bin önünde kararlı bir şekilde yürüyen Yotam giderek güçlendi.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
Yotam'ın yaptığı öbür işler, bütün savaşları ve uygulamaları, İsrail ve Yahuda krallarının tarihinde yazılıdır.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
Yotam yirmi beş yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de on altı yıl krallık yaptı.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Yotam ölüp atalarına kavuşunca, onu Davut Kenti'nde gömdüler. Yerine oğlu Ahaz kral oldu.

< 2 Nyakati 27 >