< 2 Nyakati 22 >

1 Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
Forsothe the dwelleris of Jerusalem ordeyneden Ocozie, `his leeste sone, kyng for hym; for theues of Arabeis, that felden in to the castels, hadden slayn alle the grettere `in birthe, that weren bifor hym. And Ocozie, the sone of Joram, kyng of Juda, regnede.
2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
Ocozie was of two and fourti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede o yeer in Jerusalem; the name of his modir was Athalia, the douyter of Amry.
3 Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
But he entride bi the weie of the hows of Achab; for his modir compellide hym to do yuele.
4 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
Therfor he dide yuel in the siyt of the Lord, as the hows of Achab; for thei weren counselouris to hym in to his perischyng, aftir the deth of his fadir;
5 Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
and he yede in the counsele of hem. And he yede with Joram, the sone of Achab, kyng of Israel, in to batel ayens Azahel, kyng of Sirye, in to Ramoth of Galaad. And men of Sirie woundiden Joram;
6 Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
which turnede ayen for to be heelid in Jezrahel; for he hadde take many woundis in the forseid batel. Therfor Ocozie, kyng of Juda, the sone of Joram, yede doun to visite Joram, the sone of Achab, sijk in Jezrahel;
7 Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
for it was Goddis wille ayens Ocozie, that he cam to Joram. And whanne he was comun, he yede out with hym ayens Hieu, the sone of Namsi, whom God anoyntide, that he schulde do awey the hows of Achab.
8 Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
Therfor whanne Hieu destriede the hows of Achab, he foond the princis of Juda, and the sones of the britheren of Ocozie, that `mynystriden to hym; and he killide hem.
9 Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
And he souyte thilke Ocozie, and cauyte him hid in Samarie, and after that he was brouyt to Hieu, Hieu killide hym; and thei birieden hym, for he was the sone of Josaphat, that hadde souyt God in al his herte. And noon hope was more, that ony of the generacioun of Ocozie schulde regne.
10 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
For Athalia, his modir, siy, that hir sone was deed, and sche roos, and killide alle the kyngis generacioun of the hows of Joram.
11 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
Forsothe Josabeth, the douyter of the kyng, took Joas, the sone of Ocozie, and stal hym fro the myddis of the sones of the kyng, whanne thei weren slayn; and sche hidde hym with his nurse in the closet of beddis. Forsothe Josabeth, that `hadde hid hym, was the douytir of kyng Joram, and wijf of Joiada, the bischop, and the sister of Ocozie; and therfor Athalia killide not hir.
12 Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
Therfor he was hid with hem in the hows of God sixe yeer, in whiche Athalia regnede on the lond.

< 2 Nyakati 22 >