< 2 Nyakati 15 >

1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
Et l'Esprit de Dieu descendit sur Azarias, fils d'Obed.
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
Et il sortit à la rencontre d'Asa, de Juda et de Benjamin, et il dit: Écoutez-moi, Asa, et tout Juda et Benjamin: le Seigneur est avec vous, parce que vous êtes avec lui; si vous le cherchez, vous le trouverez; si vous l'abandonnez, il vous abandonnera.
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
Il y aura bien des jours en Israël sans vrai Dieu, sans prêtre qui le révèle, sans loi.
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
Mais Dieu les convertira au Seigneur Dieu d'Israël, et il sera trouvé par eux.
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
Et, en ces jours-là, il n'y a point de paix pour agir; car un grand trouble, venant du Seigneur, est sur tous ceux qui habitent la terre.
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
Et il y aura guerre de nation à nation, de ville à ville; car Dieu les aura troublés par toutes sertes d'afflictions.
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
Fortifiez-vous donc; que vos mains ne viennent point à défaillir; car il y a une récompense pour vos œuvres.
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Après avoir entendu ces paroles et la prophétie d'Adad le prophète, le roi se fortifia, et il chassa les abominations de tout le territoire de Benjamin, et de Juda et de toutes les villes que possédait Jéroboam dans la montagne d'Ephraïm; et il fit la dédicace de l'autel du Seigneur qui était devant le temple.
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Puis, il rassembla Juda, Benjamin, les étrangers, résidant avec lui, venus d'Ephraïm, de Manassé et de Siméon; car beaucoup de ceux d'Israël s'étaient joints au roi, parce qu'ils avaient vu que le Seigneur était avec lui.
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
Et ils se réunirent à Jérusalem le troisième mois de la quinzième année du règne d'Asa.
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
Et, ce jour-là, ils sacrifièrent au Seigneur, des dépouilles qu'ils avaient ramenées, sept cents bœufs, et sept mille brebis.
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
Et ils firent alliance pour chercher le Seigneur Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme,
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
Et pour que quiconque, jeune ou vieux, homme ou femme, ne chercherait pas le Seigneur Dieu d'Israël, fût mis à mort.
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
Et ils prêtèrent serment au Seigneur à haute voix, au son des trompettes et des cors.
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
Et tout Juda se réjouit d'avoir juré, car il l'avait fait de tout son cœur, de toute son âme, et avec une pleine volonté de chercher le Seigneur; et ils le trouvèrent, et il leur donna la paix tout alentour.
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Et le roi expulsa Maacha, sa mère, pour qu'il n'y eût plus personne qui servît Astarté, et il abattit l'idole, et il la brûla dans le torrent de Cédron.
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
Néanmoins, les hauts lieux n'étaient point détruits; ils prévalaient encore en Israël; mais le cœur d'Asa fut parfait tous les jours de sa vie.
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Et il consacra de nouveau les choses saintes de David, son aïeul, et celles du temple: argent, or et vaisseaux.
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
Et il n'y eut point de guerre contre lui jusqu'à la trente-cinquième année de son règne.

< 2 Nyakati 15 >