< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
En la dix-huitième année du règne de Jéroboam, Abias commença à régner sur Juda.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Il régna trois ans à Jérusalem; et le nom de sa mère était Maacha, fille d'Uriel de Gabaon. Abias ne cessa pas d'être en guerre avec Jéroboam.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
Et il rangea en bataille une armée de quatre cent mille hommes vaillants, et Jéroboam lui en opposa huit cent mille, vaillants aussi.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Alors Abias monta sur la colline de Salomon qui est dans les montagnes d'Ephraïm, et il dit: Jéroboam, écoute-moi ainsi que tout Israël.
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
Ne devez-vous pas savoir que par une alliance sacrée, le Seigneur notre Dieu a donné pour toujours le royaume d'Israël à David et à ses fils.
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
Mais, Jéroboam, fils de Nabat, serviteur de Salomon, fils de David, s'est levé et s'est révolté contre son maître.
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
Et des hommes de pestilence, fils du péché, se sont joints à lui, qui s'est révolté contre Roboam, fils de Salomon, et Roboam, qui était jeune et d'un cœur craintif, n'osa lui tenir tête.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
Et vous maintenant, vous dites que vous résisterez au royaume du Seigneur que possèdent les fils de David; et vous êtes nombreux, et vous avez avec vous les veaux d'or qu'a faits Jéroboam, pour qu'ils soient vos dieux.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
N'avez-vous pas chassé les prêtres du Seigneur, les fils d'Aaron et les lévites? Ne vous êtes-vous point fait des prêtres parmi le peuple de toute la terre? Quiconque arrive, pour se consacrer, avec un bœuf du troupeau et sept béliers, le voilà prêtre de ce qui n'est point dieu.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
Quant à nous, nous n'avons point abandonné le Seigneur; ce sont ses prêtres, fils d'Aaron, et ses lévites qui le servent, et qui journellement
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
Offrent des holocaustes au Seigneur, matin et soir, brûlent les parfums composés, déposent sur la table pure les pains de proposition, allument à la nuit le chandelier d'or et les lampes qui doivent brûler; car, nous observons les préceptes du Seigneur Dieu de nos pères, que vous avez abandonné.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Voyez, le Seigneur et ses prêtres sont avec nous à notre tête; ce sont les trompettes sacrées qui nous donnent les signaux; fils d'Israël, gardez- vous de combattre le Seigneur, car vous ne réussirez à rien.
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
Cependant, Jéroboam ramena sur les derrières de Juda une embuscade qu'il avait dressée; il fut ainsi lui-même devant Juda, et son embuscade derrière.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
Et Juda se retournant regarda, et voilà que la bataille était devant et derrière lui; alors, il cria au Seigneur, et les prêtres sonnèrent de la trompette.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
Et les hommes de Juda crièrent, et il advint, pendant qu'ils jetaient de grands cris, que le Seigneur frappa Jéroboam et Israël devant Abias et Juda.
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
Et les fils d'Israël s'enfuirent devant Juda, et le Seigneur les livra au roi de Juda.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
Abias et son peuple les frappèrent d'une grande plaie, et cinq cent mille hommes vaillants succombèrent du côté d'Israël.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
Et, en ce jour-là, les fils d'Israël furent humiliés, et les fils de Juda prévalurent, parce qu'ils avaient espéré en Dieu.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
Abias poursuivit Jéroboam, il lui prit des villes: Béthel et ses bourgs, Mayne et ses bourgs, Ephron et ses bourgs.
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
Et Jéroboam fut sans force sous le règne d'Abias; enfin, le Seigneur le frappa, et il mourut.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
Et Abias s'affermit, et il épousa quatorze femmes, dont il eut vingt-deux fils et seize filles.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
Le reste de l'histoire d'Abias, ses actions et ses discours, sont écrits au livre du prophète Addo.

< 2 Nyakati 13 >