< 2 Nyakati 1 >

1 Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.
And Solomon the son of David was strengthened in his kingdom, and the Lord his God was with him, and magnified him to a high degree.
2 Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa.
And Solomon gave orders to all Israel, to the captains of thousands, and of hundreds, and to the rulers, and to the judges of all Israel, and the heads of the families:
3 Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani.
And he went with all the multitude to the high place of Gabaon, where was the tabernacle of the covenant of the Lord, which Moses the servant of God made, in the wilderness.
4 Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu.
For David had brought the ark of God from Cariathiarim to the place, which he had prepared for it, and where he had pitched a tabernacle for it, that is, in Jerusalem.
5 Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko.
And the altar of brass, which Beseleel the son of Uri the son of Hur had made, was there before the tabernacle of the Lord: and Solomon and all the assembly sought it:
6 Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.
And Solomon went up thither to the brazen altar, before the tabernacle of the covenant of the Lord, and offered up on it a thousand victims.
7 Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”
And behold that night God appeared to him, saying: Ask what thou wilt that I should give thee.
8 Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake.
And Solomon said to God: Thou hast shewn great kindness to my father David: and hast made me king in his stead.
9 Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi.
Now therefore, O Lord God, let thy word be fulfilled, which thou hast promised to David my father: for thou hast made me king over thy great people, which is as innumerable as the dust of the earth.
10 Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”
Give me wisdom and knowledge that I may come in and go out before thy people: for who can worthily judge this thy people, which is so great?
11 Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao,
And God said to Solomon: Because this choice hath pleased thy heart, and thou hast not asked riches, and wealth, and glory, nor the lives of them that hate thee, nor many days of life: but hast asked wisdom and knowledge, to be able to judge my people, over which I have made thee king,
12 kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”
Wisdom and knowledge are granted to thee: and I will give thee riches, and wealth, and glory, so that none of the kings before thee, nor after thee, shall be like thee.
13 Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.
Then Solomon came from the high place of Gabaon to Jerusalem before the tabernacle of the covenant, and reigned over Israel.
14 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
And he gathered to himself chariots and horsemen, and he had a thousand four hundred chariots, and twelve thousand horsemen: and he placed them in the cities of the chariots, and with the king in Jerusalem.
15 Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the king made silver and gold to be in Jerusalem as stones, and cedar trees as sycamores, which grow in the plains in great multitude.
16 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
And there were horses brought him from Egypt, and from Coa by the king’s merchants, who went, and bought at a price,
17 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha, na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
A chariot of four horses for six hundred pieces of silver, and a horse for a hundred and fifty: in like manner market was made in all the kingdoms of the Hethites, and of the kings of Syria.

< 2 Nyakati 1 >