< 1 Nyakati 29 >

1 Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana.
And king David said to all the assembly: Solomon my son, whom alone God hath chosen, is as yet young and tender: and the work is great, for a house is prepared not for man, but for God.
2 Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno.
And I with all my ability have prepared the expenses for the house of my God. Gold for vessels of gold, and silver for vessels of silver, brass for things of brass, iron for things of iron, wood for things of wood: and onyx stones, and stones like alabaster, and of divers colours, and all manner of precious stones, and marble of Paros in great abundance.
3 Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu:
Now over and above the things which I have offered into the house of my God I give of my own proper goods, gold and silver for the temple of my God, beside what things I have prepared for the holy house.
4 talanta 3,000 za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,000 za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu,
Three thousand talents of gold of the gold of Ophir: and seven thousand talents of refined silver, to overlay the walls of the temple.
5 kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”
And gold for wheresoever there is need of gold: and silver for wheresoever there is need of silver, for the works to be made by the hands of the artificers: now if any man is willing to offer, let him fill his hand today, and offer what he pleaseth to the Lord.
6 Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.
Then the heads of the families, and the princes of the tribes of Israel, and the captains of thousands, and of hundreds, and the overseers of the king’s possessions promised,
7 Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,000 na darkoni 10,000 za dhahabu, talanta 10,000 za fedha, talanta 18,000 za shaba na talanta 100,000 za chuma.
And they gave for the works of the house of the Lord, of gold, five thousand talents, and ten thousand solids: of silver ten thousand talents: and of brass eighteen thousand talents: and of iron a hundred thousand talents.
8 Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni.
And all they that had stones, gave them to the treasures of the house of the Lord, by the hand of Jahiel the Gersonite.
9 Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.
And the people rejoiced, when they promised their offerings willingly: because they offered them to the Lord with all their heart: and David the king rejoiced also with a great joy.
10 Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema: “Uhimidiwe wewe, Ee Bwana, Mungu wa Israeli baba yetu, tangu milele hata milele.
And he blessed the Lord before all the multitude, and he said: Blessed art thou, O Lord the God of Israel, our father from eternity to eternity.
11 Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana, na utukufu na enzi na uzuri, kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani ni chako wewe. Ee Bwana, ufalme ni wako; umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.
Thine, O Lord, is magnificence, and power, and glory, and victory: and to thee is praise: for all that is in heaven, and in earth, is thine: thine is the kingdom, O Lord, and thou art above all princes.
12 Utajiri na heshima vyatoka kwako; wewe ndiwe utawalaye vitu vyote. Mikononi mwako kuna nguvu na uweza ili kuinua na kuwapa wote nguvu,
Thine are riches, and thine is glory, thou hast dominion over all, in thy hand is power and might: in thy hand greatness, and the empire of all things.
13 Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu Jina lako tukufu.
Now therefore our God we give thanks to thee, and we praise thy glorious name.
14 “Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako.
Who am I, and what is my people, that we should be able to promise thee all these things? all things are thine: and we have given thee what we received of thy hand.
15 Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini.
For we are sojourners before thee, and strangers, as were all our fathers. Our days upon earth are as a shadow, and there is no stay.
16 Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako.
O Lord our God, all this store that we have prepared to build thee a house for thy holy name, is from thy hand, and all things are thine.
17 Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe.
I know my God that thou provest hearts, and lovest simplicity, wherefore I also in the simplicity of my heart, have joyfully offered all these things: and I have seen with great joy thy people, which are here present, offer thee their offerings.
18 Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako.
O Lord God of Abraham, and of Isaac, and of Israel our fathers, keep for ever this will of their heart, and let this mind remain always for the worship of thee.
19 Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”
And give to Solomon my son a perfect heart, that he may keep thy commandments, thy testimonies, and thy ceremonies, and do all things: and build the house, for which I have provided the charges.
20 Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.
And David commanded all the assembly: Bless ye the Lord our God. And all the assembly blessed the Lord the God of their fathers: and they bowed themselves and worshipped God, and then the king.
21 Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli.
And they sacrificed victims to the Lord: and they offered holocausts the next day, a thousand bullocks, a thousand rams, a thousand lambs, with their libations, and with every thing prescribed most abundantly for all Israel.
22 Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile. Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani.
And they ate, and drank before the Lord that day with great joy. And they anointed the second time Solomon the son of David. And they anointed him to the Lord to be prince, and Sadoc to be high priest.
23 Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii.
And Solomon sat on the throne of the Lord as king instead of David his father, and he pleased all: and all Israel obeyed him.
24 Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.
And all the princes, and men of power, and all the sons of king David gave their hand, and were subject to Solomon the king.
25 Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.
And the Lord magnified Solomon over all Israel: and gave him the glory of a reign, such as no king of Israel had before him.
26 Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote.
So David the son of Isai reigned over all Israel.
27 Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
And the days that he reigned over Israel, were forty years: in Hebron he reigned seven years, and in Jerusalem three and thirty years.
28 Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he died in a good age, full of days, and riches, and glory. And Solomon his son reigned in his stead.
29 Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi,
Now the acts of king David first and last are written in the book of Samuel the seer, and in the book of Nathan the prophet, and in the book of Gad the seer:
30 pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.
And of all his reign, and his valour, and of the times that passed under him, either in Israel, or in all the kingdoms of the countries.

< 1 Nyakati 29 >