< 1 Timotheo 4 >
1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
聖神明明地說:在最後的時期,有些人要背棄信德,聽信欺詐的神和魔鬼的訓言,
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
這訓言是出於那些偽善的說謊者,他們的良心已烙上了火印。
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
禁止嫁娶.戒絕一些食物;這些食物本是天主所造,叫那信仰而認識真理的人,以感恩的心所享用的;
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
因為天主所造的樣樣都好,如以感恩的心領受,沒有一樣是可擯棄的;
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
因為樣樣都是藉天主的話和祈禱祝聖了的。
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
你若拿這些提醒弟兄們,就是基督耶穌的好僕役,並顯出你在信德和你一向所追隨的好教訓上得到好的教育。
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
致於凡俗和老婦的無稽的傳說,務要躲避但要在虔敬上操練自己,
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
身體的操練益處不多,惟獨虔敬在各方面都有益處,因為有今生與來生的應許。
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
這話是確實的,值得完全接納。
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
我們勞苦奮鬥,正是如此,因為我們已寄望於永生的天主,衪是全人類,尤其是信徒們的救主。
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
你要拿這些事去指導和教訓人,
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
不要讓人小看你年輕;但要在言語行為上,在愛德、信德和潔德上,做信徒的模範。
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
直到我來時,你要專務宣讀、勤勉和教導。
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
不要疏忽心內的神恩,即從前因預言,藉長老團的覆手賜於你的神恩。
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
你要專心做這些事,全神貫注在這些事上,為使眾人看出你進步。
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
應注意你自己和你的訓言,在這些事上要堅持不變,因為你這樣做,才能救你自己,又能救你的聽眾。