< 1 Timotheo 3 >
1 Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kazi ya uangalizi, atamani kazi nzuri.
誰若想望監督的職分,是渴望一件善事:這話是確實的。
2 Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,
那麼,監督必須是是無可指摘的,只有過一個妻子的丈夫,有節制,應慎重,端莊,好客,善於教導;
3 asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.
不嗜酒,不暴戾,而應溫良和善,不貪愛錢財,
4 Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.
善於管理自己的家庭,使子女們服從,凡事端莊:
5 (Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu?)
誰若不知道管理自己的家庭.如何能照管天主的教會?
6 Asiwe mtu aliyeokoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.
不可是新奉教的,怕他妄自尊大,而陷於魔鬼所受的判決,
7 Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.
並且在外人中也必須有好聲望,怕他遭人誹謗,落入魔鬼的羅網。
8 Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.
執事也必須端莊,不一口兩舌,不飲酒過度,不貪贓;
9 Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.
以純潔的良心,保持信德的奧蹟。
10 Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.
這些人應當先受試驗,如果無瑕可指,然後才能作執事。
11 Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.
女人也必須端莊,不讒謗;有節制,凡事忠信。
12 Shemasi awe mume wa mke mmoja na inampasa aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.
執事應當只作過一個妻子的丈夫,善於管理自己子女和家庭,
13 Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Kristo Yesu.
因為善於服務的,自可獲得優越的品位,而大膽宣揚基督耶穌的信仰。
14 Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili kwamba,
我雖希望快到你那裏去,但我仍把這些事寫給你;
15 kama nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo kanisa la Mungu aliye hai, lililo nguzo na msingi wa kweli.
假使我遲遲不到,你可以知道在天主的家中應當如何行動;這家庭就是永生天主的教會,真理的柱石和基礎。
16 Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.
無不公認,這虔敬奧蹟是偉大的:就是衪出現於肉身,受證於聖神,發顯於天使,被傳於異民,見信於普世,被接於光榮。