< 1 Timotheo 2 >
1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
I exhort then, first of all, that supplications, prayers, intercessions, and giving of thanks be made for all men;
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
for kings, and all that are in authority; that we may lead a quiet and tranquil life in all godliness and propriety.
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
For this is good and acceptable in the sight of God our Saviour,
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
whose will is that all men should be saved, and come to the knowledge of the truth.
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
For there is one God, and one mediator between God and men, the man Christ Jesus,
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
who gave himself a ransom for all; to which the testimony was to be borne in its own due times,
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
whereunto I was appointed a herald and an apostle, (I speak the truth, I lie not, ) a teacher of the gentiles in faith and truth.
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
I desire, then, that the men pray in every place, lifting up holy hands, without wrath and doubting.
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
In like manner also, that women, in seemly attire, adorn themselves with modesty and sobriety, not with braided hair, and gold, or pearls, or costly apparel;
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
but, as becometh women professing godliness, with good works.
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
Let the woman learn in silence with all subjection.
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
But I suffer not the woman to teach, nor to have authority over the man, but to be in silence.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
For Adam was first formed, then Eve.
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
And Adam was not deceived; but the woman being deceived fell into transgression.
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
But she will be saved through child-bearing, if they continue in faith, and love, and holiness, with sobriety.