< 1 Timotheo 1 >
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
Paul, an apostle of Christ Jesus, through the command of God, our Saviour, and Christ Jesus, our hope,
2 Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my true child in the faith: Grace, mercy, peace, from God the Father and Christ Jesus our Lord.
3 Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo
As I besought thee, when I set out for Macedonia, to remain still in Ephesus, that thou mightst charge certain persons not to teach other doctrine,
4 wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.
nor to give heed to fables and endless genealogies, which occasion disputes rather than promote God's dispensation which is in faith, [[so I do now.]]
5 Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.
Now the end of the commandment is love, out of a pure heart and a good conscience and faith unfeigned;
6 Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,
from which some swerving turned aside to vain babbling,
7 wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.
desiring to be teachers of the Law, understanding neither what they say, nor whereof they affirm.
8 Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.
But we know that the Law is good, if a man use it lawfully,
9 Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,
knowing this, that the Law is not made for a righteous man, but for the lawless and unruly, for the ungodly and sinful, for the unholy and profane, for murderers of fathers and murderers of mothers, for man-slayers,
10 kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli,
for whoremongers, for them that defile themselves with mankind, for men-stealers, for liars, for perjured persons, and if there be any other thing that is contrary to the sound teaching,
11 ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.
according to the glorious gospel of the blessed God which was committed to my trust.
12 Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake.
And I thank him who gave me strength, Christ Jesus our Lord, that he accounted me faithful, putting me into the ministry, t
13 Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu.
though formerly I was a blasphemer, and a persecutor, and a doer of outrage; but I obtained mercy, because I did it ignorantly, in unbelief;
14 Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
and the grace of our Lord was exceedingly abundant with faith and love which is in Christ Jesus.
15 Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote.
True is the saying, and worthy of all acceptance, that Christ Jesus came into the world to save sinners, of whom I am chief.
16 Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios )
But for this cause I obtained mercy, that in me especially Christ Jesus might show forth all his long-suffering, as an example to those who should hereafter believe in him to life everlasting. (aiōnios )
17 Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
Now to the King eternal, the imperishable, invisible, only God, be honor and glory for ever and ever. Amen. (aiōn )
18 Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri,
This charge I commit to thee, my child Timothy, in accordance with the directions of the prophets before given to thee, that thou mayst in them war the good warfare,
19 ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao.
having faith, and a good conscience, which some thrusting away made shipwreck concerning the faith;
20 Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.
of whom is Hymenaeus and Alexander, whom I delivered to Satan, that they might be taught not to blaspheme.