< 1 Samweli 29 >
1 Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki, nao Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
and to gather Philistine [obj] all camp their Aphek [to] and Israel to camp in/on/with spring which in/on/with Jezreel
2 Watawala wa Wafilisti walipokuwa wakipita pamoja na vikosi vyao vya mamia na vya maelfu, Daudi na watu wake walikuwa wakitembea huko nyuma pamoja na Akishi.
and lord Philistine to pass to/for hundred and to/for thousand and David and human his to pass in/on/with last with Achish
3 Majemadari wa Wafilisti wakauliza, “Vipi kuhusu hawa Waebrania?” Akishi akajibu, “Huyu si Daudi, aliyekuwa afisa wa Sauli mfalme wa Israeli? Ameshakuwa pamoja nami kwa zaidi ya mwaka, naye tangu alipomwacha Sauli hadi sasa, sikuona kosa lolote kwake.”
and to say ruler Philistine what? [the] Hebrew [the] these and to say Achish to(wards) ruler Philistine not this David servant/slave Saul king Israel which to be with me this day or this year and not to find in/on/with him anything from day: today to fall: deserting he till [the] day: today [the] this
4 Lakini majemadari wa Wafilisti wakamkasirikia na kusema, “Mrudishe mtu huyu, apate kurudi mahali pale ulipompangia. Haimpasi kufuatana pamoja nasi vitani, asije akageuka, akawa kinyume chetu vitani. Ni kwa njia ipi bora zaidi angeweza kujipatia tena kibali kwa bwana wake, isipokuwa kwa vichwa vya watu wetu wenyewe?
and be angry upon him ruler Philistine and to say to/for him ruler Philistine to return: return [obj] [the] man and to return: return to(wards) place his which to reckon: overseer him there and not to go down with us in/on/with battle and not to be to/for us to/for Satan in/on/with battle and in/on/with what? to accept this to(wards) lord his not in/on/with head [the] human [the] they(masc.)
5 Je, huyu si ndiye Daudi walioimba kumhusu katika ngoma zao, wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
not this David which to sing to/for him in/on/with dance to/for to say to smite Saul in/on/with thousand his and David (in/on/with myriad his *Q(K)*)
6 Basi Akishi akamwita Daudi na kumwambia, “Kama vile Bwana aishivyo, wewe umekuwa mtu mwaminifu, nami ningependa utumike pamoja nami katika jeshi. Tangu siku ile uliyofika kwangu hadi sasa, sijaona kosa lolote kwako, lakini hao watawala hawakukubali.
and to call: call to Achish to(wards) David and to say to(wards) him alive LORD for upright you(m. s.) and pleasant in/on/with eye: appearance my to come out: come you and to come (in): come you with me in/on/with camp for not to find in/on/with you distress: evil from day: today to come (in): come you to(wards) me till [the] day: today [the] this and in/on/with eye: appearance [the] lord not pleasant you(m. s.)
7 Rudi na uende kwa amani; usifanye chochote cha kuwakasirisha watawala wa Kifilisti.”
and now to return: return and to go: went in/on/with peace and not to make: [do] bad: evil in/on/with eye: appearance lord Philistine
8 Daudi akamuuliza Akishi, “Lakini mimi nimefanya nini? Je, umeona nini kibaya juu ya mtumishi wako tangu siku ile niliyokuja kwako hadi leo? Kwa nini nisirudi na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
and to say David to(wards) Achish for what? to make: do and what? to find in/on/with servant/slave your from day which to be to/for face: before your till [the] day: today [the] this for not to come (in): come and to fight in/on/with enemy lord my [the] king
9 Akishi akamjibu Daudi, “Mimi ninajua ya kuwa wewe umekuwa wa kupendeza machoni pangu kama vile malaika wa Mungu. Lakini hao majemadari wa Wafilisti wamesema, ‘Huyu haimpasi kwenda vitani pamoja nasi.’
and to answer Achish and to say to(wards) David to know for pleasant you(m. s.) in/on/with eye: seeing my like/as messenger: angel God surely ruler Philistine to say not to ascend: rise with us in/on/with battle
10 Sasa amka mapema, pamoja na watumishi wa bwana wako waliofuatana nawe, nanyi ondokeni asubuhi mara kutakapopambazuka.”
and now to rise in/on/with morning and servant/slave lord your which to come (in): come with you and to rise in/on/with morning and to light to/for you and to go: went
11 Hivyo Daudi na watu wake wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda zao kurudi katika nchi ya Wafilisti, nao Wafilisti wakapanda kwenda Yezreeli.
and to rise David he/she/it and human his to/for to go: walk in/on/with morning to/for to return: return to(wards) land: country/planet Philistine and Philistine to ascend: rise Jezreel