< 1 Yohana 4 >

1 Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni.
tano nyo nob cwi ka miko kom ciyere kange yuwa tangbe no nyori kom cuwa yuwa tanngbeko kom nyimom no kwama ceri la nyo nob dukkumecwer ducce wifo mwor kalewo
2 Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu.
nyokak nyimom yuwa tongbako gwam ciya kange kiritti Almaciya bou mworon bwiyeri na kwama ce
3 Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.
no nyori yuwa tangbako ciya bo kange keritti kobo na kwamace, co yuwa tangbako, wo ko kange Almaciya kom nuwa wi botiye, kweri bi yeken wifo mwor kalewo
4 Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
kom bi beiyo curou nob kwama nine, kweri kom cam kaba diye bwiye” niworu fwer kumereu lawuro fo kalewo bidiwiyer
5 Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza.
ci na kalece dige ci toktiyeu na kalece, yilo kaleu nuwa citi
6 Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.
nyo na kwama ce, gwam ni wo nyimom kwama nurang yoti wuro kebo na kwama cemani nuwarang yoti co fiye nyo nyimom yuwa tangba keni kange yuwa tangba cwerke
7 Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
nob cwika mikko bi cwi butibi dila na kwama ce wono ki cwikadi ci bo cedi kino firen kwama, dila con nyimom kwama
8 Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo.
ni wo man ki cwi ka cwibo kwama niworo nyombo kwama, dila kwama cwika, nyo more ce ci cwika kwama cwika, nyo morece ci cwika kwama,
9 Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake.
binene kwama tomu bibwece wo nyo wine fo kalewo dige bwiye nabi bu wi cimen
10 Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.
nyo wi more curo cwika wi kebo bo bi cwi kwama dila kwama cwibe co tomu bi bweco na cok binen bwirangker lero
11 Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana.
nob cwika miko kambo kwama bi langbo nyowe daten bilang butibi
12 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
ni kange mani wo tom kwama wiye no bi cwiti bwitibiri kwama yimwi more be, dila cwika wi nyimom morebe,
13 Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake.
cofiye ba nyimom ti ciki no morebe co keneu co ki no morebe dige bwiyeu naco bo yuwa cekko
14 Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu.
bin tom bin ne bilengke biki kwama bi bwece, na yilam nii fuloka kale
15 Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
gwam niwo ciya kiritti bi bwe kwama ri kwama yim morece co kene co mwor kwama
16 Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu. Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake.
bin nyimom bin ne bilengke cwi ka kwama woru mabinen tiye, kwama cwika, wa yim mwor cwikari yim mwor cwika kwama, kwama la yim mworece
17 Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.
nyo no wurori cwika kwama fiyam fiye yime tiber kumet nakom yimki nyomka kambo ken kibi diye warka, kambo co no curo nyie, bona curoken wimwor kalewo
18 Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.
twai mani mwor cwika la cwika kendo bouti ki twai, dige bwiye twaiyo ken kange warka dila niwo ki twaiyeu manki cwika ko ken
19 Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza.
bi cwi bileng lati dige bwiye kwama ten maka cwika beke
20 Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona?
no nika tok ki ci cwi kwama tiri la ci ko kecetiri nii cwerke, tano niwo cwibo kece wuroci totiyeri, mani ce cwikwama wuro mani cototiyeti
21 Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.
wuro co kero nyo cike ci mone, gwam niwo cwi kwama tiye tam nyo ca bilang yice,

< 1 Yohana 4 >