< 1 Wakorintho 7 >

1 Basi kuhusu mambo yale mliyoyaandika: Ni vyema mwanaume asimguse mwanamke.
La dor dikero wo kom mulnag meneu, “Yori kabo nii a kere nawiye.”
2 Lakini ili kuepuka zinaa, kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.
Dila ker cuwakatini dor bwiratum, daten nii a yilam ki wice ri nawiye ken a yilam ki bwece.
3 Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe, naye vivyo hivyo mke kwa mumewe.
Bwayileu daten a ne wice dikero wo yilam na wice ceu nyo nawiye ama bwecenen tiye ken.
4 Mwanamke hana mamlaka juu ya mwili wake bali mumewe, wala mume hana mamlaka juu ya mwili wake bali mkewe.
Na wiyeu man ki bikwan keret dor bwiceronen, la bwece cike. Nyo ken nii luweu mani ki bikwan keret dor bwicero nin. dila wice cike.
5 Msinyimane, isipokuwa mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda fulani ili mweze kujitoa kwa maombi, kisha mrudiane tena ili Shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kutokuwa na kiasi.
Kom kwak re bwiti wabkanka, no kebo wo kom ciya cuko bwiti kom nawo kumenin bi duware. kom ma wuro na kom neken dor kumero duloh. la nakom wab kangi wari tak, kati tila bwe kelkeleu cuwa komti bwini taka dorek kumeko.
6 Nasema haya kama ushauri na si amri.
Dila mi yikom wuro na neka yulanek kebo na werfun ni ce.
7 Laiti watu wangekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa kipawa chake kutoka kwa Mungu, mmoja ana kipawa cha namna hii na mwingine ana cha namna ile.
Man cwi nubo gwam yilam na mo. Dila kwama nerangbo luma nereko kidimen-kidimen. kange ki wang luma nereko wo kange ce wang ko wurendo.
8 Kwa wale wasiooa na kwa wajane, nasema hivi, ingekuwa vizuri wasioe.
Ki nubo buro nabeu kange natubo nabarub cebo bwiyameu, miki an yor cinen ciya nare na mo.
9 Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe na kuolewa, kwa maana ni afadhali kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa.
Dila no mani ci ya dol taka dorek tiri, ciya narangum. An la cinen diker ciya narangum kange wo kuruu a tum ci tiyeu.
10 Kwa wale waliooana nawapa amri (si mimi ila ni Bwana): Mke asitengane na mumewe.
ki nubo wo narangumeu ma neci werfundo woti kebo mo, la Tee kwama- Na wiye a kubo kubore lo bwece.
11 Lakini akitengana, ni lazima akae bila kuolewa, ama sivyo apatane tena na mumewe. Wala mume asimpe mkewe talaka.
Dila no cin kubo bwece nin ri, ca nare kange nii kebo nyori, ca ywel kangum tibercero kange bwece, Nii nabareu a yware wice.
12 Lakini kwa wengine nasema (si Bwana ila ni mimi): Kama ndugu ana mke asiyeamini, naye huyo mke anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache.
La ki tangnumbo miki, mo kebo Tee kwama no kange nii wi ki nawiye wo nebo bilenkeri, no nawiyeu co ciya can yim kange cori, ca ywaco re.
13 Naye mwanamke aaminiye kama ameolewa na mwanaume asiyeamini na huyo mume anakubali kuishi naye, basi huyo mwanamke asimwache.
no nawiye wiki bwece wo nebo bilenkeri no bwece co ciya can yim kange cori ca dob core.
14 Kwa maana huyo mume asiyeamini anatakaswa kupitia mkewe, naye mke asiyeamini anatakaswa kupitia mumewe anayeamini. Kama isingalikuwa hivyo watoto wenu wangalikuwa si safi, lakini ilivyo sasa wao ni watakatifu.
wori, Nii nabareu wo nebo bilenkeu yilam wo cii cokcokeu ker wicer, la nawiye wo nebo bilenkeu yilam wo cii cokcokeu ker bwecer. kebo nyori, bibeyo lokumeu mani a yila ti wucak. Dila kibi com ciin cokumcii coke.
15 Lakini kama yule asiyeamini akijitenga, basi afanye hivyo. Katika hali kama hiyo mwanamke au mwanaume aaminiye hafungwi, kwa sababu Mungu ametuita tuishi kwa amani.
Dila no buro bilenkeu curi, dom co a yaken ti no bwi nawori, noro wo nii nabareu teweu kaka nawiyeu, mani dor cer kwama cobo nabi yi mor fuwor neret.
16 Wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mumeo? Au wewe mume unajuaje kama utamwokoa mkeo?
Mwa nyom nyi, mo nawiye keno mwan ceer bwe meri? kaka mwa nyom nyi bwayile keno mwan ceer wimweri?
17 Lakini kila mtu na aishi maisha aliyopangiwa na Bwana, yale Mungu aliyomwitia. Hii ni sheria ninayoiweka kwa makanisa yote.
Bwenno nyiri, kambo kwama nerangbo dikeor yilam be ki dimeneu, nii a ma nangen do kambo kwama cou cew. wuro werfun miir ki bi kurwabero nin gwam.
18 Je, mtu alikuwa tayari ametahiriwa alipoitwa? Asijifanye asiyetahiriwa. Je, mtu alikuwa hajatahiriwa alipoitwa? Asitahiriwe.
Kange wi wo biyen biye lar fiya co cii cwo cou naci ne belenke? ca dore naci yilam na nii biye bo lareu. kamnge wi wo biye bo lar ki kwamawo cicwo co mor bilenke? ca biye re lar cero.
19 Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu. Lakini kuzitii amri za Mungu ndilo jambo muhimu.
Biye ka larek kange bwini biyeka larek keb diker kwomkak. Dikero dateneu neak durek ki werfun
20 Basi kila mmoja wenu na abaki katika hali aliyoitwa nayo.
Nii a titi mor bicoro cii couceu. Fiyaco kwama cwo co naci ne bilenkeu.
21 Je, wewe ulipoitwa ulikuwa mtumwa? Jambo hilo lisikusumbue. Ingawaje unaweza kupata uhuru, tumia nafasi uliyo nayo sasa kuliko wakati mwingine wowote.
Mwin changa fiyaco kwama cwo nena? kwom de dor mwer dor cer. Dila no mwan fiya nure ceer kari, mani nyo.
22 Kwa maana yeyote aliyeitwa katika Bwana akiwa mtumwa yeye ni mtu huru kwa Bwana, kama vile yeyote aliyekuwa huru alipoitwa yeye ni mtumwa wa Kristo.
Wori nii wo kwama cuo co fiyaco cin cangau fiya ceerka kwama nin. Nyo tak, nii wo kebo canga fiyaco kwama cuo co nanci ne bilenkeu, canga Almasiya.
23 Mlinunuliwa kwa gharama; msiwe watumwa wa wanadamu.
Cii teen kum ki kener ducce, nyori kom yilam de canga nobeb.
24 Ndugu zangu, kama kila mtu alivyoitwa, akae katika wito wake alioitiwa na Mungu.
Kebmibo, bwenno nii fiya dor cero mor ye fiyaco ci cuo co naci ne bilenke ri, bi yilare kwama nen bwin.
25 Basi, kuhusu wale walio bikira, mimi sina amri kutoka kwa Bwana, lakini mimi natoa shauri kama mtu ambaye ni mwaminifu kwa rehema za Bwana.
dor nubo buro narangum bo wiyeu, ma mamni ki werfun kwama nen. Dila maki tok dikero mato daten ne na nii wo ki cii bwini kwamak, lan ciya ka.
26 Kwa sababu ya shida iliyoko kwa sasa, naona ni vyema mkibaki kama mlivyo.
Matori ker kungka nerek ko you tiyeu, yori kabo nii a yilam nawo ci yimeu.
27 Je, umeolewa? Basi usitake talaka. Je, hujaoa? Usitafute mke.
Mwi bwam ki duka naka nawiye? dore ywaka cek. No mwi manki nawiyeri, dore naka nawiyek.
28 Lakini kama ukioa, hujatenda dhambi; na kama bikira akiolewa, hajatenda dhambi. Lakini wale wanaooa watakabiliana na matatizo mengi katika maisha haya, nami nataka kuwazuilia hayo.
Dila no mwin nam ri, mwi mabo bwirang ke, no bubiya wo nambo wiyeu nam di, ci mabo bwirang ke. Dila buro narangumeu an nuwarang dotange tini ki denmwer-Kidemen, la ma cwiti nami cok kom more ce.
29 Lakini ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama wasio na wake;
Dila wo miki, kembibo kang kene ko da dum cuka, tabti na wo, yaken cuko kab, nubo ki natubeu a yi namwi cii man cuko.
30 nao wanaoomboleza, kama ambao hawaombolezi; wenye furaha kama wasiokuwa nayo; wale wanaonunua, kama vile vitu walivyonunua si mali yao;
Nubo ci wiye tiyeu a mani namwi kebo nubo ci wiye, kange buro ma bilangtum tiyeu namwi kebo nubo ma bilang tum tiye, Nubo tenang diker tiyeu namwi cii man ki diker.
31 nao wale wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama ambao hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inapita.
nubo buro ma nangenti ki kale weu a mare namwi ciin neken bikwan ceer maka nangenek ki kaleu, wori wank kale kowo atii dim.
32 Ningetaka msiwe na masumbufu. Mwanaume ambaye hajaoa anajishughulisha na mambo ya Bwana, jinsi ya kumpendeza Bwana.
Ma cwi nakom fiya ceerka ki komka tini. Nii wo na beu, ki bulnag ki diker yilam Tee kwama ce, kambo a ciya ti kange ce.
33 Lakini mwanaume aliyeoa anajishughulisha na mambo ya dunia, jinsi ya kumfurahisha mkewe,
Dila nii wo na meu ki kwama dikero dor bitinenereu kambo ci lunga neer wicero tiyeu.
34 na mawazo yake yamegawanyika. Mwanamke asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana: lengo lake ni awe mtakatifu kimwili na kiroho. Lakini yule aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia, jinsi atakavyoweza kumfurahisha mumewe.
Neer cero tikangum. Nawiye wo nabeu kaka'a bubiya ki kwa'a diker yilam kwama ce, kambo ca neken dorceroti bwi kange yuwa tangbe. Dila nawiye nameu ki kwom dor dikero kale neu, kambo bwece a nuwa luma cek tiyeu.
35 Ninasema haya kwa faida yenu wenyewe, sio ili kuwawekea vizuizi bali mpate kuishi kwa jinsi ilivyo vyema bila kuvutwa pengine katika kujitoa kwenu kwa Bwana.
Ma tok wuro na tikang kom, kemi nan dok kom totange. ma tok wuro ki dikero yor-yore, na kom neken dor kumero Tee kwama nin kambo diker kange mani a kwom kom tiye.
36 Kama mtu yeyote anadhani kwamba hamtendei ilivyo sawa mwanamwali ambaye amemposa, naye akiwa umri wake unazidi kuendelea na mtu huyo anajisikia kwamba inampasa kuoa, afanye kama atakavyo. Yeye hatendi dhambi. Yawapasa waoane.
Dila no kange kwati ki mani ci ma bubiya conin dikero dateneri, no bubiyau cum cor nakar, takeu no tam nyori, ca ma dike ci cwi tiyeu. Kebo bwirangke ca matiye. Cii ya kangum.
37 Lakini mwanaume ambaye ameamua moyoni mwake kutooa bila kulazimishwa na mtu yeyote, bali anaweza kuzitawala tamaa zake kutomwoa huyo mwanamwali, basi anafanya ipasavyo.
Dila no cin tiim kibi kwan ner cerdi no kwom cobo catin tom dor cerori, no cin tum mor nenerce can ma wuro ri, na ci yomre bubiyace ri, can mani yora.
38 Hivyo basi, mwanaume amwoaye mwanamwali afanya vyema, lakini yeye asiyemwoa afanya vyema zaidi.
La co nii wo nam bubiyaceu mani dong dong, tak ri, wuro ciya ki mani ca na'a bubiya cetiyeu mani la kece ceu yorak.
39 Mwanamke aliyeolewa amefungwa na sheria maadamu mumewe yu hai. Lakini mumewe akifa, basi mwanamke huyo yuko huru kuolewa na mume mwingine ampendaye, lakini lazima awe katika Bwana.
Bolangko bwam na wiyeu ki kwama wo bwece ki dumeu, Dila no bwece bwiyamri, cin tin nam kange nii wo ca cwitiyeu, la a yilam mor nubo lo Tee kwama.
40 Lakini kwa maoni yangu, angekuwa na furaha zaidi akibaki alivyo. Nami nadhani pia nina Roho wa Mungu.
Duwal mor warkemiu, catin nuwa luma duce no ci yiken kambo ci yimmeri, takeu mi kwatiri mo ken man wiki yuwa tangbe kwama.

< 1 Wakorintho 7 >