< 1 Wakorintho 5 >

1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
Olen kuulnud mitmelt poolt, et teie keskel on sugukõlvatust, ja veel sellist kõlvatust, mida ei esine isegi paganate seas, et keegi magab oma isa naisega.
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
Ja teie olete veel uhked! Te peaksite pigem leinama ja endi keskelt eemaldama mehe, kes seda on teinud.
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
Kuigi ma olen ihulikult eemal, olen ma vaimus kohal. Ja sel moel teie juures viibides teinud otsuse meie Issanda Jeesuse nimel selle üle, kes on seda teinud.
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
Kui te olete kokku tulnud ja mina olen teiega vaimus ja meie Issanda Jeesuse vägi on kohal,
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
andke see mees saatana kätte ihu hävitamiseks, et tema vaim võiks pääseda Issanda päeval.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
Teie kiitlemine on kohatu! Kas te siis ei tea, et pisut juuretist paneb käärima kogu taigna?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Puhastage end vanast juuretisest, et te oleksite uus taigen, hapnemata, nagu te ju tegelikult oletegi. Sest ka meie paasatall Kristus on tapetud.
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
Pidutsegem siis siiruse ja tõe hapnemata leivaga, mitte aga vana leivaga, mis on hapendatud kurjuse ja tigedusega!
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
Ma kirjutasin teile oma kirjas, et te ei teeks tegemist sugukõlvatutega,
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
sugugi mitte mõeldes selle maailma kõlvatuid, ahneid ja riisujaid või ebajumalateenijaid, sest muidu tuleks teil maailmast üldse ära minna.
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
Ma tahtsin öelda, et te ei teeks tegemist ühegagi, kes nimetab end vennaks või õeks, kristlaseks, kuid on sugukõlvatu, ahne, ebajumalateenija, laimaja, joodik või riisuja. Sellisega ärge isegi koos sööge!
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
Sest kas minu asi on mõista kohut nende üle, kes on kogudusest väljas? Kas te ei peaks kohut mõistma nende üle, kes on koguduses?
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
Väljas olijate üle mõistab kohut Jumal. Heitke kurjad välja eneste keskelt!

< 1 Wakorintho 5 >