< 2 Wakorintho 1 >
1 Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
Paulus, Kristuse Jeesuse apostel Jumala tahtel, ja vend Timoteos, Korintoses olevale Jumala kogudusele ja kõigile Ahhaias asuvaile Jumala pühadele:
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Armu ja rahu teile Jumalalt, meie Isalt, ning Issandalt Jeesuselt Kristuselt!
3 Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
Kiidetud olgu Jumal, meie Issanda Jeesuse Kristuse Isa, halastuse Isa, kõige lohutuse Jumal.
4 Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
Tema lohutab meid igas meie ahistuses, et meie omakorda võiksime lohutada neid, kes on mis tahes ahistuses lohutusega, mida me saame Jumalalt.
5 Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
Sest nii nagu me oleme osalised rohketes Kristuse kannatustes, nõnda saame me ka rohkesti lohutust Kristuse kaudu.
6 Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
Kui nüüd meid ahistatakse, siis sünnib see teie julgustuseks ja päästmiseks. Ja kui meid julgustatakse, siis sünnib see teie julgustuseks nende samade kannatuste talumises, mida meiegi kannatame.
7 Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
Ja meie lootus teile on kindel, sest me teame, et nii nagu te olete saanud osa meie kannatustest, saate osa ka meie lohutusest.
8 Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
Me ei taha, vennad ja õed, et teile jääks teadmata, millist ahistust me Aasia provintsis kogesime. Meid rõhuti nii rängalt üle meie jõu, nii et me ei lootnud pääseda eluga.
9 Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
Tõepoolest, tundsime, et meile on langetatud surmaotsus. Ent see õpetas meid lootma mitte eneste peale, vaid Jumala peale, kes surnud üles äratab.
10 Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
Tema päästis meid sellest surmavast ohust ja päästab uuesti. Tema peale oleme lootnud, et ta päästab ka edaspidi,
11 Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
kui ka teie meie eest palvetades appi tulete. Siis paljud tänavad Jumala käest tulnud armuanni eest, mis anti meile paljudele palvetele vastates.
12 Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
Meie kiitlemine on see: meie südametunnistus kinnitab, et me oleme elanud selles maailmas, ja eriti suhetes teiega, jumalikus pühaduses ja siiruses. Seda oleme me teinud mitte ilmalikus tarkuses, vaid Jumala armus.
13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
Me ei kirjuta teile midagi sellist, mida te ei suudaks lugeda ega mõista. Ma loodan,
14 kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
et kui te seni olete meid mõistnud vaid osaliselt, siis te jõuate ka täieliku mõistmiseni, nõnda et te võite Issanda Jeesuse päeval kiidelda meist, nagu meie kiitleme teist.
15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
Selle usaldusega ma kavatsesin tulla esiteks teie juurde, et te saaksite teistkordselt armu,
16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
ja teie kaudu jätkata teed Makedooniasse ja Makedooniast tulla tagasi teie juurde ning lasta teil mind saata teele Juudamaale.
17 Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
Selline oli mu plaan. Kas ma toimisin kergemeelselt? Või teen ma oma plaane meelt muutes, öeldes kõigepealt „jah-jah“, ja siis „ei-ei“?
18 Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
Kuid Jumal on ustav, nii et meie kõne teile ei ole ühtaegu „jah“ja „ei“.
19 Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
Sest Jumala Poeg Jeesus Kristus, keda meie – mina, Siilas ja Timoteos – oleme teie seas kuulutanud, ei olnud ühtaegu „jah“ja „ei“, vaid temas on alati olnud „jah“.
20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
Sest nii palju kui on Jumala tõotusi, on Jeesuses „jah“neile kõigile. Seepärast ütleme meiegi tema abiga „aamen!“Jumala kiituseks.
21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
Jumal on see, kes on kinnitanud meid koos teiega Kristusesse. Tema on meid võidnud
22 kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
ja oma pitseriga märgistanud ning andnud oma Vaimu pandi meie südamesse.
23 Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
Olgu Jumal mulle tunnistajaks minu hinge juures, et teie säästmise pärast jätsin ma Korintosesse tulemata.
24 Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.
Me ei taha valitseda teie usu üle, sest usus te püsite niigi, vaid me töötame koos teiega, et te võiksite olla rõõmsad.