< 1 Wakorintho 15 >

1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
A oznajmiam wam, bracia, ewangelię, którą wam głosiłem, a którą przyjęliście i w której trwacie;
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
Przez którą też dostępujecie zbawienia, jeśli pamiętacie to, co wam głosiłem, chyba że uwierzyliście na próżno.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
Najpierw bowiem przekazałem wam to, co i ja otrzymałem, że Chrystus umarł za nasze grzechy, zgodnie z Pismem;
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
Że został pogrzebany, że zmartwychwstał trzeciego dnia, zgodnie z Pismem;
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
I że ukazał się Kefasowi, a potem tym dwunastu.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
Potem ukazał się więcej niż pięciuset braciom naraz, z których większość żyje aż dotąd, a niektórzy zasnęli.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
Potem ukazał się Jakubowi, potem wszystkim apostołom.
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
A ostatniemu ze wszystkich ukazał się i mnie, jak poronionemu płodowi.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
Ja bowiem jestem najmniejszym z apostołów i nie jestem godny nazywać się apostołem, bo prześladowałem kościół Boży.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
Lecz z łaski Boga jestem tym, czym jestem, a jego łaska względem mnie nie okazała się daremna, ale pracowałem więcej od nich wszystkich, jednak nie ja, lecz łaska Boga, która [jest] ze mną.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
Czy więc ja, czy oni, tak głosimy i tak uwierzyliście.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
A jeśli się o Chrystusie głosi, że został wskrzeszony z martwych, jak [mogą] niektórzy pośród was mówić, że nie ma zmartwychwstania?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
Jeśli bowiem nie ma zmartwychwstania, to i Chrystus nie został wskrzeszony.
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
A jeśli Chrystus nie został wskrzeszony, to daremne [jest] nasze głoszenie, daremna też wasza wiara.
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
I okazuje się, że jesteśmy fałszywymi świadkami Boga, bo świadczyliśmy o Bogu, że wskrzesił Chrystusa, którego nie wskrzesił, jeśli umarli nie są wskrzeszani.
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
Jeśli bowiem umarli nie są wskrzeszani, to i Chrystus nie został wskrzeszony.
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
A jeśli Chrystus nie został wskrzeszony, daremna [jest] wasza wiara i nadal jesteście w swoich grzechach.
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
Tak więc i ci, którzy zasnęli w Chrystusie, poginęli.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
Jeśli tylko w tym życiu mamy nadzieję w Chrystusie, jesteśmy ze wszystkich ludzi najbardziej nieszczęśliwi.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
Tymczasem jednak Chrystus został wskrzeszony z martwych i stał się pierwszym plonem tych, którzy zasnęli.
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
Skoro bowiem śmierć [przyszła] przez człowieka, przez człowieka [przyszło] też zmartwychwstanie umarłych.
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
Jak bowiem w Adamie wszyscy umierają, tak też w Chrystusie wszyscy zostaną ożywieni.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
Ale każdy w swojej kolejności, Chrystus jako pierwszy plon, potem ci, którzy należą do Chrystusa, w [czasie] jego przyjścia.
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
A potem będzie koniec, gdy przekaże królestwo Bogu i Ojcu, gdy zniszczy wszelką zwierzchność oraz wszelką władzę i moc.
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
Bo on musi królować, aż położy wszystkich wrogów pod swoje stopy.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
A ostatni wróg, który zostanie zniszczony, to śmierć.
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
Wszystko bowiem poddał pod jego stopy. A gdy mówi, że wszystko jest [mu] poddane, [jest] jasne, że oprócz tego, który mu wszystko poddał.
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
Gdy zaś wszystko zostanie mu poddane, wtedy i sam Syn będzie poddany temu, który mu poddał wszystko, aby Bóg był wszystkim we wszystkich.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
Bo inaczej co zrobią ci, którzy przyjmują chrzest za zmarłych, jeśli umarli w ogóle nie są wskrzeszani? Po co przyjmują chrzest za zmarłych?
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
Po co i my każdej godziny narażamy się na niebezpieczeństwo?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
[Zapewniam was] przez chlubę, którą mam z was w Jezusie Chrystusie, naszym Panu, że każdego dnia umieram.
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
Jeśli na sposób ludzki walczyłem z bestiami w Efezie, jaki z tego mam pożytek, jeśli umarli nie są wskrzeszani? Jedzmy i pijmy, bo jutro pomrzemy.
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Nie łudźcie się. Złe rozmowy psują dobre obyczaje.
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
Ocknijcie się ku sprawiedliwości i nie grzeszcie; niektórzy bowiem nie mają poznania Boga. Mówię to ku waszemu zawstydzeniu.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
Lecz powie ktoś: Jak umarli są wskrzeszani i w jakim ciele przychodzą?
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
Głupcze! To, co siejesz, nie ożyje, jeśli nie obumrze.
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
I to, co siejesz, to nie ciało, które ma powstać, ale gołe ziarno, na przykład pszeniczne lub jakieś inne.
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
Bóg zaś daje mu ciało, jakie chce, a każdemu z ziaren właściwe jemu ciało.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
Nie każde ciało jest jednakowe, ale inne jest ciało ludzi, a inne ciało zwierząt, inne ryb, a inne ptaków.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
Są też ciała niebieskie i ciała ziemskie, lecz inna jest chwała [ciał] niebieskich, a inna ziemskich.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
Inna chwała słońca, inna chwała księżyca, a inna chwała gwiazd. Gwiazda bowiem od gwiazdy różni się jasnością.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
Tak też jest ze zmartwychwstaniem umarłych. Sieje się [ciało] w zniszczalności, a jest wskrzeszane w niezniszczalności;
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
Sieje się w niesławie, a jest wskrzeszane w chwale, sieje się w słabości, a jest wskrzeszane w mocy;
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
Sieje się ciało cielesne, a jest wskrzeszane ciało duchowe. Jest ciało cielesne, jest też ciało duchowe.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
Tak też jest napisane: Stał się pierwszy człowiek, Adam, duszą żyjącą, [a] ostatni Adam duchem ożywiającym.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
Jednak pierwsze nie jest to, co duchowe, ale to, co cielesne, potem duchowe.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
Pierwszy człowiek z ziemi – ziemski, drugi człowiek – [sam] Pan z nieba.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
Jaki jest ten ziemski, tacy i ziemscy; a jaki jest niebieski, tacy i niebiescy.
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
A jak nosiliśmy obraz ziemskiego, tak będziemy nosili obraz niebieskiego.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
To zaś mówię, bracia, że ciało i krew nie mogą odziedziczyć królestwa Bożego ani to, co zniszczalne, nie odziedziczy tego, co niezniszczalne.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
Oto oznajmiam wam tajemnicę: Nie wszyscy zaśniemy, ale wszyscy będziemy przemienieni;
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
W jednej chwili, w mgnieniu oka, na ostatnią trąbę. Zabrzmi bowiem [trąba], a umarli zostaną wskrzeszeni niezniszczalni, a my zostaniemy przemienieni.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
To bowiem, co zniszczalne, musi przyodziać się w to, co niezniszczalne, a to, co śmiertelne, przyoblec się w nieśmiertelność.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
A gdy to, co zniszczalne, przyoblecze się w niezniszczalność, a to, co śmiertelne, przyoblecze się w nieśmiertelność, wtedy wypełni się to słowo, które [jest] napisane: Połknięta jest śmierć w zwycięstwie.
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs g86)
Gdzież [jest], o śmierci, twoje żądło? Gdzież jest, o piekło, twoje zwycięstwo? (Hadēs g86)
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
Żądłem zaś śmierci [jest] grzech, a siłą grzechu prawo.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Lecz dzięki [niech będą] Bogu, który nam dał zwycięstwo przez naszego Pana Jezusa Chrystusa.
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
A tak, moi mili bracia, bądźcie stali, niezachwiani, zawsze obfitujący w dziele Pana, wiedząc, że wasza praca nie jest daremna w Panu.

< 1 Wakorintho 15 >