< 2 Wakorintho 1 >
1 Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
Paweł, z woli Boga apostoł Jezusa Chrystusa, i Tymoteusz, brat, do kościoła Bożego, który jest w Koryncie, ze wszystkimi świętymi, którzy są w całej Achai.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Łaska wam i pokój od Boga, naszego Ojca, i Pana Jezusa Chrystusa.
3 Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
Błogosławiony [niech będzie] Bóg i Ojciec naszego Pana Jezusa Chrystusa, Ojciec miłosierdzia i Bóg wszelkiej pociechy;
4 Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
Który nas pociesza w każdym naszym utrapieniu, abyśmy i my mogli pocieszać tych, którzy są w jakimkolwiek ucisku, taką pociechą, jaką sami jesteśmy pocieszani przez Boga.
5 Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
Jak bowiem w nas obfitują utrapienia Chrystusa, tak też przez Chrystusa obfituje nasza pociecha.
6 Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
Jeśli więc doznajemy ucisku – [to] dla waszego pocieszenia i zbawienia, które sprawia, że znosicie te same utrapienia, które i my cierpimy; i jeśli doznajemy pociechy – [to] dla waszego pocieszenia i zbawienia.
7 Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
A nasza nadzieja co do was [jest] mocna, bo wiemy, że jak jesteście uczestnikami utrapienia, tak i pociechy.
8 Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
Nie chcemy bowiem, bracia, abyście nie wiedzieli o ucisku, który nas spotkał w Azji, że byliśmy obciążeni ponad miarę [i] ponad siły, tak że zaczęliśmy wątpić, czy przeżyjemy.
9 Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
Więcej, sami w sobie mieliśmy wyrok śmierci, abyśmy nie ufali samym sobie, lecz Bogu, który wskrzesza umarłych.
10 Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
On to wyrwał nas z tak wielkiej śmierci i [jeszcze] wyrywa. W nim [też] mamy nadzieję, że nadal będzie wyrywać;
11 Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
Także przy waszej pomocy poprzez modlitwę za nas, aby dar, który [otrzymaliśmy] dzięki wielu, stał się dla wielu powodem dziękczynienia za nas.
12 Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
To bowiem jest naszą chlubą: świadectwo naszego sumienia, że w prostocie i w szczerości Bożej, nie w cielesnej mądrości, ale w łasce Boga postępowaliśmy na świecie, a szczególnie względem was.
13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
Nie piszemy wam [nic] innego, jak tylko to, co czytacie albo rozumiecie. Spodziewam się zaś, że też do końca zrozumiecie;
14 kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
Jak już po części nas zrozumieliście, że jesteśmy waszą chlubą, jak i wy naszą w dniu Pana Jezusa.
15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
Z tą ufnością chciałem przybyć do was wcześniej, abyście otrzymali powtórne dobrodziejstwo;
16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
A od was udać się do Macedonii, a z Macedonii znowu przybyć do was i zostać przez was wyprawionym do Judei.
17 Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
Czy więc tak postanawiając, postąpiłem lekkomyślnie? Albo [czy] to, co postanawiam, postanawiam według ciała, aby było u mnie „tak, tak” i „nie, nie”?
18 Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
Lecz [jak] Bóg jest wierny, tak nasze słowa do was nie były „tak” i „nie”.
19 Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
Ponieważ Syn Boży, Jezus Chrystus, który wśród was głoszony był przez nas, [to znaczy] przeze mnie, Sylwana i Tymoteusza, nie był „tak” i „nie”, lecz było w nim „tak”.
20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
Ile jest bowiem obietnic Boga, w nim [są] „tak” i w nim [są] „Amen”, ku chwale Boga przez nas.
21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
Tym zaś, który utwierdza nas [razem] z wami w Chrystusie i który nas namaścił, [jest] Bóg;
22 kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
Który też zapieczętował nas i dał do naszych serc Ducha [jako] zadatek.
23 Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
A ja wzywam Boga na świadka mojej duszy, że aby was oszczędzić, nie przybyłem dotąd do Koryntu.
24 Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.
Nie dlatego, że panujemy nad waszą wiarą, ale jesteśmy pomocnikami waszej radości; wiarą bowiem stoicie.