< 1 Wakorintho 14 >

1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
Higer efter Kærligheden, og tragter efter de aandelige Gaver, men mest efter at profetere.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
Thi den, som taler i Tunger, taler ikke for Mennesker, men for Gud; thi ingen forstaar det, men han taler Hemmeligheder i Aanden.
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
Men den, som profeterer, taler Mennesker til Opbyggelse og Formaning og Trøst.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
Den, som taler i Tunger, opbygger sig selv; men den, som profeterer, opbygger en Menighed.
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Men jeg ønsker, at I alle maatte tale i Tunger, men endnu hellere, at I maatte profetere; den, som profeterer, er større end den, som taler i Tunger, med mindre han udlægger det, for at Menigheden kan faa Opbyggelse deraf.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
Men nu, Brødre! dersom jeg kommer til eder og taler i Tunger, hvad vil jeg da gavne eder, hvis jeg ikke taler til eder enten ved Aabenbaring eller ved Kundskab, enten ved Profeti eller ved Lære?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Selv de livløse Ting, som give Lyd, være sig en Fløjte eller en Harpe, naar de ikke gøre Skel imellem Tonerne, hvorledes skal man saa kunne forstaa, hvad der spilles paa Fløjten eller Harpen?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
Ja, ogsaa naar en Basun giver en utydelig Lyd, hvem vil da berede sig til Krig?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
Saaledes ogsaa med eder: dersom I ikke ved Tungen fremføre tydelig Tale, hvorledes skal man da kunne forstaa det, som tales? I ville jo tale hen i Vejret.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
Der er i Verden, lad os sige, saa og saa mange Slags Sprog, og der er intet af dem, som ikke har sin Betydning.
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
Dersom jeg nu ikke kender Sprogets Betydning, bliver jeg en Barbar for den, som taler, og den, som taler, bliver en Barbar for mig.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Saaledes ogsaa med eder: naar I tragte efter aandelige Gaver, da lad det være til Menighedens Opbyggelse, at I søge at blive rige derpaa!
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
Derfor, den, som taler i Tunger, han bede om, at han maa kunne udlægge det.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
Thi dersom jeg taler i Tunger og beder, da beder vel min Aand, men min Forstand er uden Frugt.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
Hvad da? Jeg vil bede med Aanden, men jeg vil ogsaa bede med Forstanden; jeg vil lovsynge med Aanden, men jeg vil ogsaa lovsynge med Forstanden.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Ellers, naar du priser Gud i Aanden, hvorledes vil da den, som indtager den uindviedes Plads, kunne sige sit Amen til din Taksigelse, efterdi han ikke ved, hvad du siger?
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
Thi vel er din Taksigelse smuk, men den anden opbygges ikke.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
Jeg takker Gud for, at jeg mere end I alle taler i Tunger.
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
Men i en Menighed vil jeg hellere tale fem Ord med min Forstand, for at jeg ogsaa kan undervise andre, end ti Tusinde Ord i Tunger.
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Brødre! vorder ikke Børn i Forstand, men værer Børn i Ondskab, i Forstand derimod vorder fuldvoksne!
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
Der er skrevet i Loven: „Ved Folk med fremmede Tungemaal og ved fremmedes Læber vil jeg tale til dette Folk, og de skulle end ikke saaledes høre mig, siger Herren.‟
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
Saaledes er Tungetalen til et Tegn, ikke for dem, som tro, men for de vantro; men den profetiske Gave er det ikke for de vantro, men for dem, som tro.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
Naar altsaa den hele Menighed kommer sammen, og alle tale i Tunger, men der kommer uindviede eller vantro ind, ville de da ikke sige, at I rase?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
Men dersom alle profetere, og der kommer nogen vantro eller uindviet ind, da overbevises han af alle, han bedømmes af alle,
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
hans Hjertes skjulte Tanker aabenbares, og saa vil han falde paa sit Ansigt og tilbede Gud og forkynde, at Gud er virkelig i eder.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Hvad da, Brødre? Naar I komme sammen, da har enhver en Lovsang, en Lære, en Aabenbaring, en Tungetale, en Udlægning; alt ske til Opbyggelse!
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
Dersom nogen taler i Tunger, da være det to, eller i det højeste tre hver Gang, og den ene efter den anden, og een udlægge det!
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
Men dersom der ingen Udlægger er til Stede, da tie hin i Menigheden, men han tale for sig selv og for Gud!
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
Men af Profeter tale to eller tre, og de andre bedømme det;
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
men dersom en anden, som sidder der, faar en Aabenbarelse, da tie den første!
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
Thi I kunne alle profetere, den ene efter den anden, for at alle kunne lære, og alle blive formanede,
32 Roho za manabii huwatii manabii.
og Profeters Aander ere Profeter undergivne.
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
Thi Gud er ikke Forvirringens, men Fredens Gud. Ligesom i alle de helliges Menigheder
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
skulle eders Kvinder tie i Forsamlingerne; thi det tilstedes dem ikke at tale, men lad dem underordne sig, ligesom ogsaa Loven siger.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
Men ville de lære noget, da adspørge de deres egne Mænd hjemme; thi det er usømmeligt for en Kvinde at tale i en Menighedsforsamling.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
Eller er det fra eder, at Guds Ord er udgaaet? eller er det til eder alene, at det er kommet?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
Dersom nogen tykkes, at han er en Profet eller aandelig, han erkende, at hvad jeg skriver til eder, er Herrens Bud.
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
Men er nogen uvidende derom, saa faar han være uvidende!
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
Altsaa, mine Brødre! tragter efter at profetere og forhindrer ikke Talen i Tunger!
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
Men alt ske sømmeligt og med Orden!

< 1 Wakorintho 14 >