< 1 Nyakati 5 >

1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Isarel e camin teh Reuben e capanaw katang doeh. Hateiteh, a na pa e ikhun a khin sak dawkvah, camin lah a onae hah Isarel e capa Joseph e capanaw koe poe e lah ao. Hatdawkvah, setouknae dawk camin lah a onae hah pakhum e lah awm hoeh.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Judah teh a hmaunawnghanaw hlak a tha a sai teh, ahni dawk hoi kaukkung a tâco. Camin lah a onae teh Joseph ni a coe.
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Isarel camin Reuben e casaknaw teh Hanok, Pallu, Hezron hoi Karmi.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
Joel casak teh, a capa Shemaiah, Shemaiah capa Gog, Gog capa Shimei.
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Shimei capa Maikah, Mikah capa Reaiah, Reaiah capa Baal.
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Baal capa Beerah. Ahni teh Reuben e khobawi lah ao eiteh, Assyria siangpahrang Tiglathpileser ni san lah a hrawi.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Amae a nawngha Jeiel hoi Zekhariah, ahnimouh roi teh ca catoun separuinae pakhumnae dawkvah, imthungnaw kahrawikung lah ao.
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Azaz capa Bela, Shema capa Azaz, Joel capa Shema ni Aroer hoi Nebo Baalmeon totouh kho a sak.
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
Kanîtholah Euphrates palang hoi kahrawng thung kâennae totouh, a coe awh. Bangkongtetpawiteh, Gilead ram dawk saringnaw hah a pungdaw toe.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Sawl se navah Hagri miphunnaw hoi a kâtuk awh teh, Gilead kanîtholah totouh, rimnaw dawk kho a sak awh.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Gad e casaknaw teh avangvanglah Bashan ram dawk Salkah totouh ao awh.
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Bashan vah a lû lah Joel, apâhni lah Shapham, Janai hoi Shaphat tinaw doeh.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
A na pa imthung hoi a hmaunawnghanaw Michael, Meshullam, Sheba, Jorai, Jakhan, Zia, Eber hoi sari touh a pha awh.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
Hetnaw teh Huri capa Abihail e capanaw doeh. Ahni teh Jaorah capa doeh. Gilead capa, Michael capa, Jeshishai capa, Jahdo capa, Buz capa lah ao.
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Guni capa, Abdiel capa, Ahni teh imthung kahrawikung lah ao.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
Hatdawkvah, Gilead hoi Bashan khotenaw tengpam e ram pueng khori totouh kho a sak awh.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Hote hnonaw pueng teh, Judah siangpahrang Jotham e se hoi Isarel siangpahrang Jeroboam e se teh setouknae dawk thut lah ao toe.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
Reuben casak, Gad casak, hoi Manasseh miphun tangawn dawk hoi tarankahawinaw, bahling, tahloi ka patuem thai e naw, likathoumnaw, taran ka tuk thai e naw 44, 760 touh a pha awh.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
Hatnavah, Hagri, Jetur, Naphish hoi Nodabnaw hoi a kâtuk awh.
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
Kâtuk nahaiyah Cathut koe a hram awh teh, ama a kâuep awh dawkvah, ahnimouh teh a kabawp awh. Hatdawkvah, Hagrinaw hoi ahnimouh koe kaawm e abuemlah a kut dawk hoi a rungngang awh.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
Saringnaw a man pouh awh teh, kalauk 50000, tu 250000, hoi la 2000 hoi tami 100000 a la awh.
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
Tarantuknae teh Cathut e lah ao dawkvah, tami moikapap a due awh. San toung totouh a onae hmuen koe ao awh.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Manasseh miphun tangawn teh, haw e ram dawk kho a sak awh. Bashan hoi Baalhermon hoi Senir hoi Hermon mon totouh tami teh a pungdaw awh.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
Hetnaw heh a imthungnaw kahrawikung lah a o: Epher, Ishi, Eliel, Azriel, Jeremiah, Hodaviah, Jahdiel. Ahnimanaw teh tami a thakaawme, min kamthang e, imthung kahrawikung lah ao awh.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Mintoenaw e Cathut koe yuemkamcu awh hoeh dawkvah, ahnimae hmaitung Cathut ni a raphoe teh, hote ram dawk e cathutnaw koe a kâyo awh.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
Hottelah Isarel Cathut ni Assiria siangpahrang Pul, Assiria siangpahrang Tiglathpileser e lungthin a tho sak teh, Reuben hoi Gad, Manasseh miphun tangawn hah san lah a man awh teh, Halah, Habor, Hara tinaw hah Gozan palang a ceikhai awh teh atu totouh ao awh.

< 1 Nyakati 5 >