< 1 Crónicas 26 >
1 La distribución de los porteros fue así: de los coreítas, Meselemías, hijo de Coré, de los hijos de Asaf.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Meselemías tuvo hijos: Zacarías el primogénito, Jediael el segundo, Zebadías el tercero, Jatniel el cuarto,
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elam el quinto, Johanán el sexto, Elioenai el séptimo.
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 También Obed-edom tuvo hijos: Semaías el primogénito, Jozabad el segundo, Joa el tercero, Sacar el cuarto, Natanael el quinto;
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Amiel el sexto, Isacar el séptimo y Peultai el octavo, porque ʼElohim lo bendijo.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 También a su hijo Semaías le nacieron hijos que fueron jefes en sus casas paternas, porque eran varones valientes y esforzados.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Los hijos de Semaías: Otni, Rafael, Obed, Elzabad, y sus hermanos, hombres esforzados; también Eliú y Samaquías.
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Todos éstos fueron de los hijos de Obed-edom, ellos con sus hijos y sus hermanos, hombres robustos y fuertes para el servicio: 62, de Obed-edom.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Los hijos de Meselemías y sus hermanos: 18 hombres valientes.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 También Hosa, uno de los hijos de Merari, tuvo hijos: Simri el jefe. Aunque no era el primogénito, su padre lo colocó de jefe,
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Hilcías el segundo, Tebalías el tercero, Zacarías el cuarto. Todos los hijos de Hosa y sus hermanos fueron 13.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Entre éstos se hizo la distribución de los porteros, y se alternaban los principales de los varones en la guardia con sus hermanos, para ministrar en la Casa de Yavé.
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Echaron suertes para cada puerta: el pequeño con el grande, según sus casas paternas.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 La suerte para la oriental cayó a Selemías. Metieron en las suertes a Zacarías su hijo, consejero entendido. La suerte suya salió para la del norte.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 Para Obed-edom la puerta del sur, y a sus hijos la casa de provisiones del Templo.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Para Supim y Hosa, la del occidente, junto a la puerta de Salequet, en el camino de la subida. Guardia con guardia se correspondían.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Al oriente seis levitas, al norte cuatro de día, al sur cuatro de día, y en los almacenes de dos en dos.
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 En el patio, al occidente, cuatro en el camino, y dos en el mismo patio.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Tales fueron las distribuciones de los porteros de los hijos de Coré y de Merari.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 De los levitas, Ahías estaba encargado de los tesoros de la Casa de ʼElohim y de los tesoros de las cosas consagradas.
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Los hijos de Laadán, los hijos de los gersonitas de Laadán, es decir, los jehielitas, eran los jefes de las casas paternas de Laadán gersonita.
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Los hijos de Jehieli, Zetam y Joel su hermano, estaban a cargo de los tesoros de la Casa de Yavé.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 De entre los amramitas, de los izharitas, de los hebronitas y de los uzielitas:
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 Sebuel, hijo de Gersón, hijo de Moisés, era jefe de los tesoros.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 En cuanto a su hermano Eliezer, cuyo hijo era Rehabías, del cual fue hijo Jesaías, hijo de éste Joram, cuyo hijo era Zicri, del cual fue hijo Selomit.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Este Selomit y sus hermanos estaban a cargo de todos los tesoros y de todas las cosas sagradas que el rey David, los jefes de las casas paternas, junto con los jefes de millares y de centenas y jefes del ejército,
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 consagraron de las guerras y del botín para el mantenimiento de la Casa de Yavé.
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 Estaba a cargo de Selomit y sus hermanos todo lo que consagró el vidente Samuel, Saúl, hijo de Cis, Abner, hijo de Ner, y Joab, hijo de Sarvia. [También estaba a su cargo] todo lo que cualquiera consagraba.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 En cuanto a los izharitas, Quenanías y sus hijos fueron encargados de la administración externa de Israel como oficiales y jueces.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 Con respecto a los hebronitas, Hasabías y sus hermanos, 1.600 hombres valientes, fueron asignados para los negocios de Israel al occidente del Jordán, de toda la obra de Yavé y del servicio del rey.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 El año 40 del reinado de David Jerías era el jefe de los hebronitas según sus generaciones por sus casas paternas. Entre ellos fueron hallados hombres de extraordinario valor en Jazer de Galaad.
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Sus hermanos, hombres valientes, eran 2.700 jefes de casas paternas. El rey David los constituyó [como] oficiales de los rubenitas, los gaditas y la media tribu de Manasés, para todas las cosas de ʼElohim y todo asunto del rey.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.