< 1 Crónicas 23 >
1 Cuando David era anciano y lleno de días, proclamó a su hijo Salomón como rey sobre Israel.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 Reunió a todos los jefes de Israel, con los sacerdotes y levitas.
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 Fueron contados los levitas de 30 años arriba. El número de ellos, contados uno por uno, fue 38.000.
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 De éstos, 24.000 debían supervisar la obra de la Casa de Yavé, y 6.000 debían ser funcionarios y jueces.
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 4.000 eran porteros y 4.000 alababan a Yavé con los instrumentos que yo hice para tributar alabanzas, dijo David.
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 Los repartió David en grupos según los hijos de Leví: Gersón, Coat y Merari.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Los hijos de Gersón: Laadán y Simei.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Los hijos de Laadán, tres: Jehiel el primero, después Zetam y Joel.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Los hijos de Simei, tres: Selomit, Haziel y Harán. Éstos fueron los jefes de las casas paternas de Laadán.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 Los hijos de Simei: Jahat, Zina, Jeús y Bería. Estos cuatro fueron los hijos de Simei.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 Jahat era el primero, y Zina el segundo. Pero Jeús y Bería no tuvieron muchos hijos, por lo cual fueron contados como una sola familia.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel, ellos cuatro.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Los hijos de Amram: Aarón y Moisés. Aarón fue apartado para que se dedicara con sus hijos a las cosas más sagradas, quemaran incienso delante de Yavé, ministraran y bendijeran en su Nombre para siempre.
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 Los hijos de Moisés, varón de ʼElohim, fueron contados en la tribu de Leví.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Los hijos de Moisés: Gersón y Eliezer.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Sebuel, hijo de Gersón, fue el jefe.
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 Rehabías, hijo de Eliezer, fue el jefe. Eliezer no tuvo otros hijos, pero los hijos de Rehabías se multiplicaron grandemente.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 El hijo de Izhar fue Selomit, el jefe.
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Los hijos de Hebrón: Jerías el primero, Amarías el segundo, Jahaziel el tercero, y Jecamán el cuarto.
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Los hijos de Uziel: Micaía el primero, e Isías el segundo.
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Los hijos de Merari: Mahli y Musi. Hijos de Mahli: Eleazar y Cis.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 Eleazar murió y no tuvo hijos, sino solo hijas, de modo que sus parientes, los hijos de Cis, las tomaron como esposas.
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Los hijos de Musi fueron tres: Mahli, Edar y Jeremot.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Éstos fueron los hijos de Leví según sus casas paternas, jefes de casas paternas según el censo de ellos, contados por sus nombres, individualmente, de 20 años arriba, los cuales trabajaban en el ministerio de la Casa de Yavé.
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 Porque David dijo: Yavé ʼElohim de Israel dio paz a su pueblo Israel. Él morará en Jerusalén para siempre.
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 Además los levitas ya no tendrán que cargar el Tabernáculo y todos los utensilios para su ministerio.
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 Así que, conforme a las últimas palabras de David, los hijos de Leví fueron contados de 20 años arriba.
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Estaban bajo las órdenes de los hijos de Aarón a fin de que ministraran en la Casa de Yavé en los patios y las cámaras: para la purificación de toda cosa consagrada, la obra del ministerio de la Casa de ʼElohim
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 y los Panes de la Presencia, mantener la flor de harina destinada al sacrificio, a las hojuelas sin levadura, a lo preparado en sartén, a lo tostado y a toda medida y cuenta,
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 asistir cada mañana todos los días a dar gracias y tributar alabanzas a Yavé, y asimismo al llegar la noche,
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 ofrecer todos los holocaustos a Yavé todos los sábados, las lunas nuevas y las solemnidades señaladas continuamente delante de Yavé, según el número fijado por la ordenanza que los prescribe,
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 y para que tuvieran la custodia del Tabernáculo de Reunión y del Santuario, bajo las órdenes de sus hermanos hijos de Aarón en el ministerio de la Casa de Yavé.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.