< Salmos 126 >

1 Una canción de ascensos. Cuando Yahvé hizo volver a los que regresaron a Sión, éramos como los que sueñan.
Wimbo wa kwenda juu. Bwana alipowarejeza mateka Sayuni, tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2 Entonces se nos llenó la boca de risa, y nuestra lengua con el canto. Entonces dijeron entre las naciones, “Yahvé ha hecho grandes cosas por ellos”.
Vinywa vyetu vilijaa kicheko, ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe. Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa, “Bwana amewatendea mambo makuu.”
3 Yahvé ha hecho grandes cosas por nosotros, y nos alegramos.
Bwana ametutendea mambo makuu, nasi tumejaa furaha.
4 Restablece nuestra suerte, Yahvé, como los arroyos del Néguev.
Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa, kama vijito katika Negebu.
5 Los que siembran con lágrimas cosecharán con alegría.
Wapandao kwa machozi watavuna kwa nyimbo za shangwe.
6 El que sale llorando, llevando semilla para sembrar, ciertamente volverá con alegría, llevando sus gavillas.
Yeye azichukuaye mbegu zake kwenda kupanda, huku akilia, atarudi kwa nyimbo za shangwe, akichukua miganda ya mavuno yake.

< Salmos 126 >