< Proverbios 1 >
1 Los proverbios de Salomón, hijo de David, rey de Israel:
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2 para conocer la sabiduría y la instrucción; para discernir las palabras del entendimiento;
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
3 para recibir instrucción en el trato sabio, en la rectitud, la justicia y la equidad;
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
4 para dar prudencia a los simples, conocimiento y discreción al joven —
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5 para que el sabio escuche y aumente su aprendizaje; para que el hombre de entendimiento alcance el sano consejo;
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6 para entender un proverbio y parábolas, las palabras y acertijos de los sabios.
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7 El temor a Yahvé es el principio del conocimiento, pero los necios desprecian la sabiduría y la instrucción.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8 Hijo mío, escucha la instrucción de tu padre, y no abandones las enseñanzas de tu madre;
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9 pues serán una guirnalda que adornará tu cabeza, y cadenas alrededor del cuello.
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10 Hijo mío, si los pecadores te atraen no lo consienten.
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
11 Si dicen: “Ven con nosotros. Acechemos la sangre. Acechemos en secreto a los inocentes sin causa.
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
12 Que se los trague vivos como el Seol, y entero, como los que bajan a la fosa. (Sheol )
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol )
13 Encontraremos toda la riqueza valiosa. Llenaremos nuestras casas con el botín.
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
14 Echarán su suerte entre nosotros. Todos tendremos un bolso”—
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
15 hijo mío, no camines por el camino con ellos. Mantén tu pie fuera de su camino,
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
16 porque sus pies corren hacia el mal. Se apresuran a derramar sangre.
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
17 Porque la red se tiende en vano a la vista de cualquier ave;
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
18 pero estos acechan su propia sangre. Acechan en secreto por sus propias vidas.
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
19 Así son los caminos de todo aquel que tiene afán de lucro. Le quita la vida a sus dueños.
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
20 La sabiduría llama en voz alta en la calle. Ella pronuncia su voz en las plazas públicas.
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
21 Llama a la cabeza de los lugares ruidosos. A la entrada de las puertas de la ciudad, pronuncia sus palabras:
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
22 “¿Hasta cuándo, simples, amaréis la sencillez? Cuánto tiempo se deleitarán los burladores en la burla, ¿y los tontos odian el conocimiento?
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
23 Vuélvete ante mi reprimenda. Mira, derramaré mi espíritu sobre ti. Te daré a conocer mis palabras.
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
24 Porque te he llamado y te has negado; He extendido mi mano y nadie me ha hecho caso;
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25 pero has ignorado todos mis consejos, y no quería ninguna de mis reprimendas;
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26 Yo también me reiré de tu desastre. Me burlaré cuando la calamidad te alcance,
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27 cuando la calamidad te alcanza como una tormenta, cuando tu desastre llega como un torbellino, cuando la angustia y la angustia se apoderan de ti.
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
28 Entonces me llamarán, pero no responderé. Me buscarán con ahínco, pero no me encontrarán,
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29 porque odiaban el conocimiento, y no eligió el temor a Yahvé.
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30 No querían ningún consejo mío. Despreciaron toda mi reprimenda.
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31 Por eso comerán del fruto de su propio camino, y se llenan de sus propios esquemas.
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
32 Porque la reincidencia de los simples los matará. La despreocupación de los tontos los destruirá.
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
33 Pero el que me escuche habitará con seguridad, y estarán tranquilos, sin temor a sufrir daños”.
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”