< Proverbios 2 >

1 Hijo mío, si recibes mis palabras, y guardad mis mandamientos en vuestro interior,
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 para que vuelvas tu oído a la sabiduría, y aplica tu corazón a la comprensión;
kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 sí, si se llama al discernimiento, y levanta tu voz para que te entiendan;
na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
4 si la buscas como plata, y buscarla como a los tesoros escondidos;
na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 entonces entenderás el temor de Yahvé, y encontrar el conocimiento de Dios.
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
6 Porque Yahvé da sabiduría. De su boca sale el conocimiento y la comprensión.
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 Él acumula la sana sabiduría para los rectos. Es un escudo para los que caminan con integridad,
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 para que guarde los caminos de la justicia, y preservar el camino de sus santos.
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9 Entonces entenderás la rectitud y la justicia, la equidad y todo buen camino.
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
10 Porque la sabiduría entrará en tu corazón. El conocimiento será agradable para tu alma.
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11 La discreción velará por ti. La comprensión te mantendrá,
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
12 para librarte del camino del mal, de los hombres que hablan cosas perversas,
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
13 que abandonan los caminos de la rectitud, para andar por los caminos de la oscuridad,
wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
14 que se alegran de hacer el mal, y se deleitan en la perversidad del mal,
wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
15 que son torcidos en sus caminos, y descarriados en sus caminos,
ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
16 para librarte de la mujer extraña, incluso de la extranjera que halaga con sus palabras,
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
17 que abandona al amigo de su juventud, y olvida el pacto de su Dios;
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
18 por su casa lleva a la muerte, sus caminos a los espíritus difuntos.
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
19 Ninguno de los que van a ella regresa, ni alcanzan los caminos de la vida.
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
20 Por lo tanto, camina por el camino de los hombres buenos, y guarda los caminos de los justos.
Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
21 Porque los rectos habitarán la tierra. Lo perfecto permanecerá en él.
Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
22 Pero los malvados serán eliminados de la tierra. Los traidores serán desarraigados de ella.
Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

< Proverbios 2 >