< Salmos 45 >

1 Para el director del coro. Al son de “los lirios”. Un salmo (masquil) de los hijos de Coré. Un canto de amor. Fui movido a escribir sobre esto. Déjame compartir lo que he escrito para el rey. Lo que diré viene de la pluma de un hábil escritor.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 Eres más guapo que cualquier otro. Siempre hablas con tanta gracia, porque Dios te ha bendecido.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 ¡Agita tu espada, gran guerrero! ¡Cabalga poderoso en gloria y majestad!
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 en tu camino majestuoso a la victoria, en defensa de la verdad, la humildad, y lo correcto, porque eres fuerte y puedes actuar de forma poderosa.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Tus flechas perforan los corazones de tus enemigos; las naciones caen a tus pies.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Tu trono viene de Dios, y permanecerá para siempre. El cetro con el que gobiernas es un cero de justicia.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 Tú amas lo que está bien y aborreces o malo. Por eso es que Dios, tu Dios, te ha puesto por encima de todos al ungirte con el aceite de la victoria.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 Tus mantos son perfumados con aloe, mirra y casia; te hace feliz la música que es tocada en instrumentos de cuerda en hermosos palacios decorados con marfil.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 Entre las mujeres nobles están las hijas del rey; la reina permanece detrás de ti en tu lado derecho, llevando joyería echa con oro refinado de Ofir.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Escucha lo que tengo que decirte, hija; presta atención, por favor. Olvídate de tu pueblo y tu familia.
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 Que el rey te desea por tu hermosura; respétalo, porque él es tu Señor.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 El pueblo de Tiro vendrá con regalos; la gente rica buscará tu favor.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 Dentro de su preparación, la princesa luce hermosa con su vestido de oro.
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 Vistiendo sus hermosas ropas ella es traída al rey, seguida por sus damas de honor.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 ¡Qué procesión tan feliz y alegre entra al palacio del rey!
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Tus hijos tomarán el lugar de tu padre; como princesa los harás gobernadores sobre la tierra.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 Por mis palabras serás famosa a través de las generaciones, y las naciones te adorarán para siempre.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

< Salmos 45 >