< Job 36 >

1 Elihú continuó hablando.
Elihu akaendelea kusema:
2 “Ténganme un poco más de paciencia y déjenme explicarles. Todavía tengo algo que decir en nombre de Dios.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Compartiré mis amplios conocimientos, y demostraré que mi Creador tiene razón.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Les aseguro que lo que digo no son mentiras, pues soy un hombre cuyos conocimientos son de primer orden.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Dios es poderoso, pero no desprecia a nadie; es poderoso en fuerza y comprensión.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 No mantiene vivo al impío, sino que hace justicia al oprimido.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Siempre presta atención a los que hacen el bien, y los coloca en tronos con los reyes, honrándolos eternamente.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Si están encadenados, atados con cuerdas de sufrimiento,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 entonces les explica lo que han hecho: sus pecados arrogantes.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Les hace prestar atención y les ordena que dejen de pecar.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 “Si escuchan y hacen lo que Dios dice, vivirán su vida con felicidad.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Pero si no escuchan, tendrán una muerte violenta, ignorantes de Dios.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Los que rechazan a Dios se aferran a su amargura. Incluso cuando él los disciplina, no claman a él por ayuda.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Mueren en su juventud; su vida termina entre los hombres que se prostituyen en el templo.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 A través del sufrimiento, Dios salva a los que sufren; consigue su atención a través de sus problemas.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 “Dios está tratando de rescatarte de las fauces de los problemas a un lugar de libertad y seguridad, llenando tu mesa con los mejores alimentos.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Pero tú te preocupas por la suerte de los malvados; el juicio y la justicia llenan tu mente.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Pero ten cuidado de que tu cólera no te seduzca en la burla; y no dejes que el tamaño del ‘soborno’ te conduzcan al pecado.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 ¿Tu grito de auxilio te sostendrá cuando vengan los problemas?
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 No anheles la noche en la que las personas son arrebatadas repentinamente.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 ¡Cuida que no te vuelvas al mal! Porque es por esto que estás siendo probado a través del sufrimiento.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 “¡Mira qué poder tiene Dios! ¿Qué maestro es como él?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 ¿Quién le ha enseñado lo que debe hacer? ¿Quién puede decirle: ‘Has hecho mal’?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Al contrario, alábenle por lo que ha hecho, como dicen los cantos.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Todo el mundo ha visto la creación de Dios, aunque sólo desde la distancia.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 “Mira qué grande es Dios, más de lo que podemos entender. Nadie puede contar sus años.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Él extrae el agua y la destila en rocío y lluvia.
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Las nubes derraman lluvia, cayendo abundantemente sobre la humanidad.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 ¿Alguien puede entender cómo se extienden las nubes, o cómo ruge el trueno desde donde vive?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Mira cómo esparce los rayos a su alrededor, y cubre de oscuridad las profundidades del mar.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Con estas acciones gobierna a los pueblos, les proporciona abundante alimento.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Tiene el rayo en sus manos y ordena dónde debe caer.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 El trueno anuncia su presencia: hasta el ganado sabe cuándo se avecina una tormenta”.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >