< Job 28 >

1 “Hay minas de plata y lugares donde se refina el oro.
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 El hierro se extrae de la tierra y el cobre se funde a partir de su mineral.
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Los mineros llevan lámparas a la oscuridad del subsuelo y buscan el mineral hasta donde pueden llegar en las sombras y la penumbra.
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 Cavan una mina lejos de donde vive la gente o lejos de donde la gente pueda pasar. Se agarran de cuerdas que cuelgan en las fosas.
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 El pan sale de la tierra, pero debajo parece que el fuego le ha dado la vuelta.
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 Aquí las rocas contienen lapislázuli y el polvo contiene oro.
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 Ningún ave de rapiña puede ver estos caminos, ningún ojo de halcón puede percibir.
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 Ninguna fiera ha pasado por ese camino; el león no ha andado por allí.
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 Los mineros atacan la dura roca; derriban las raíces de las montañas.
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 Hacen túneles en la roca, buscando cuidadosamente cada piedra preciosa.
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 Ponen diques en las fuentes de los ríos, y sacan a la luz lo que está oculto.
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 “Pero, ¿dónde se puede encontrar la sabiduría? ¿Dónde está el lugar para obtener el entendimiento?
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Los seres humanos no conocen el camino de la sabiduría; no se encuentra entre los vivos.
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Las aguas profundas dicen: ‘No está aquí’, y el mar dice: ‘Tampoco está aquí’.
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 No se puede comprar con oro ni con plata.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Su valor no se puede medir, ni siquiera con el oro de Ofir; es más precioso que el ónix o el lapislázuli.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 El oro o el cristal fino no se pueden comparar con la sabiduría; no se puede cambiar por joyas de oro.
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 El coral y el cristal no son dignos de mención; el precio de la sabiduría está muy por encima de los rubíes.
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 El topacio de Etiopía no se puede comparar con ella; ni se puede comprar con el oro más puro.
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 “Entonces, ¿de dónde viene la sabiduría? ¿Dónde se adquiere el entendimiento?
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 La sabiduría está oculta de la vista de todos los seres vivos, incluso las aves del cielo no pueden verla.
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Abadón y la Muerte dice: ‘Sólo hemos oído un rumor sobre ella’.
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 “Sólo Dios comprende el camino de la sabiduría; él sabe dónde se encuentra.
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 Porque él mira hasta el final de la tierra; ve todo lo que hay bajo el cielo.
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 Él decidió cuál sería la fuerza del viento y reguló las aguas.
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 Fijó el límite de la lluvia e hizo un camino para el rayo.
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 Luego consideró la sabiduría. La examinó, le dio su aprobación y la declaró buena.
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 Dijo a los hombres: ‘Reverenciar al Señor es la sabiduría, y apartarse del mal es el entendimiento’”.
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”

< Job 28 >