< Rimljanom 9 >
1 Resnico govorim v Kristusu, ne lažem, to mi spričuje moja vest v duhu svetem,
Nasema ukweli katika Kristo. Sisemi uongo, na dhamira yangu hushuhudia pamoja nami katika Roho Mtakatifu,
2 Da imam veliko žalost in neprenehano bolečino v svojem srcu.
kwamba kuna huzuni kubwa na maumivu yasiyo koma ndani ya moyo wangu.
3 Kajti želel bi, da bi bil sam jaz preklet od Kristusa za svoje brate, kteri so mi v rodu po mesu;
Kwamba ningetamani mimi mwenyewe kulaaniwa na kutengwa mbali na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, wale wa jamii yangu katika mwili.
4 Kteri so Izraelci, kterih je posinstvo, in slava, in zaveze, in postavodajstvo, in služba, in obljube,
Wao ni Waisraeli. Walio na hali ya kufanyika watoto, wa utukufu, wa maagano, na zawadi ya sheria, kumwabudu Mungu, na ahadi.
5 Kteri so očetje, in od kterih je Kristus po mesu, kteri je Bog nad vsemi blagoslovljen na veke. Amen. (aiōn )
Wao ni watangulizi ambako Kristo amekuja kwa heshima kuvaa mwili huu - ambaye yeye ni Mungu wa vyote. Naye asifiwe milele. Amina. (aiōn )
6 Ni pa tako, da je beseda Božja izgubljena, ker niso vsi ti Izraelci, kteri so od Izraela.
Lakini si kwamba ahadi za Mungu zimeshindwa kutimia. Maana si kila mtu aliye Israeli ni Mwiisraeli halisi.
7 Tudi kteri so seme Abrahamovo, niso vsi otroci, nego: "Izaku se ti bo imenovalo seme."
Sivyo hata kwa uzao wa Abrahamu kuwa ni watoto wake halisi. Lakini, “ni kupitia Isaka uzao wako utaitwa.”
8 To je, niso ti, kteri so otroci mesa, otroci Božji, nego otroci obljube računijo se za seme.
Hii ni kwamba, watoto wa mwili si watoto wa Mungu. Lakini watoto wa ahadi wanatazamwa kuwa kama uzao.
9 Kajti beseda obljube je ta: "Ta čas bom prišel in Sara bo imela sina."
Maana hili ndilo neno la ahadi: “Katika majira haya nitakuja, na Sara atapewa mtoto.”
10 Pa ne samo ona, nego tudi Rebeka, z enim imajoč otroke, z Izakom očetom našim;
Si hili tu, lakini baada ya Rebeka kupata mimba kwa mtu mmoja, Isaka baba yetu-
11 Kajti ko se še nista narodila, tudi ne storila kaj dobrega ali hudega, da bi ostal sklep Božji poleg izbire,
kwamba watoto walikuwa bado hawajazaliwa na alikuwa hajafanya jambo lolote zuri au baya, ili kwamba kusudi la Mungu kulingana na uchaguzi lisimame, wala si kwa matendo, lakini ni kwa sababu ya yule aitae.
12 Ne za voljo del, nego za voljo tistega, kteri kliče, reklo se jej je: "Veči bo služil manjšemu."
Ilinenwa kwake, “Mkubwa atamtumikia mdogo.”
13 Kakor je pisano: "Jakoba sem ljubil, a Ezava sovražil."
Kama ilivyo kwisha andikwa: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Kaj torej porečemo? krivica je pri Bogu? Bog ne daj!
Basi tena tutasema nini? Je kuna udhalimu kwa Mungu? La hasha.
15 Kajti Mojzesu govori: "Pomiloval bom, kogar pomilujem, in usmilil se ga bom, kogar se usmiljujem."
Kwa kuwa anasema kwa Musa, “nitakuwa na rehema kwa yule nitakayemrehemu, na nitakuwa na huruma kwa yule nitakayemhurumia.”
16 To torej ni v moči ne tega, kteri hoče, ne tega, kteri ne če, nego Boga, kteri pomiluje.
Kwa hiyo basi, si kwa sababu ya yeye atakaye, wala si kwa sababu ya yeye ambaye hukimbia, lakini kwa sababu ya Mungu, ambaye huonesha rehema.
17 Kajti pismo govori Faraonu: "Za to sem te obudil, da pokažem na tebi svojo moč, in da se oznani moje ime po vsej zemlji."
Kwa kuwa maandiko husema kwa Farao, “Kwa kusudi hili maalumu nilikuinua, ili kwamba nioneshe nguvu zangu katika wewe, na ili kwamba jina langu litangazwe katika nchi yote.”
18 Tako torej, kogar hoče, pomiluje, a kogar hoče, trdi.
Hivyo basi, Mungu huwa na rehema kwa yeyote ampendaye, na kwa ambaye humpenda, humfanya kuwa mkaidi.
19 Porečeš mi torej; kaj se še toži? kdo njegovej volji nasprotuje?
Kisha utasema kwangu, “Kwa nini bado anaona kosa? Ni yupi ambaye alikwisha kustahimili matakwa yake?”
20 Ali kdo si ti, o človek, kteri se z Bogom pregovarjaš? poreče li izdelek izdelovalcu: za kaj si me naredil tako?
Kinyume chake, mwanadamu, wewe ni nani ujibue kinyume na Mungu? Kuna uwezekano wowote wa kilichofinyangwa kusema kwa mfinyanzi, “Kwanini ulinifanya hivi mimi?”
21 Nima li oblasti lončar nad glino, da iz ravno tiste grude naredi eno posodo za čast, a drugo za nečast?
Je mfinyazi huwa hana haki juu ya udongo kutengeneza chombo kwa matumizi maalumu kutokana na bonge lile lile, na chombo kingine kwa matumizi ya kila siku?
22 Če je Bog hotel pokazati jezo in razglasiti svojo moč, prenesel je v velikej potrpljivosti posode jeze pripravljene za pogubo.
Vipi kama Mungu, ambaye ana utayari wa kuonesha gadhabu yake na kufanya nguvu yake kujulikana, alistahimili kwa uvumilivu wa kutosha vyombo vya gadhabu vilivyoandaliwa kwa kuangamiza?
23 In da bi razglasil bogastvo slave svoje na posodah usmiljenja, ktere je naprej pripravil za zlavo,
Vipi kama alifanya hivi ili kwamba aoneshe wingi wa utukufu wake juu ya vyombo vya rehema, ambavyo alikwisha kuviandaa kwa ajili ya utukufu?
24 Ktere nas je tudi poklical ne samo izmed Judov, nego tudi izmed poganov;
Vipi kama alifanya hii pia kwetu, ambaye pia alituita, si tu kutoka kwa Wayahudi, lakini pia kutoka kwa watu wa Mataifa?
25 (Kakor tudi pri Oseji pravi: "Imenoval bom ne moje ljudstvo svoje ljudstvo, in ne ljubico ljubico."
Kama asemavyo pia katika Hosea: “Nitawaita watu wangu ambao hawakuwa watu wangu, na mpendwa wake ambaye hakupendwa.
26 In bode, na mestu, kjer se jim je reklo: "Niste moj narod vi, tam se bodo imenovali sinovi Boga živega."
Na itakuwa kwamba pale iliposemwa kwao, 'Ninyi si watu wangu,' pale wataitwa 'wana wa Mungu aliye hai.”'
27 Izaija pa vpije nad Izraelom: "Ko bi bilo število sinov Izraelovih kolikor morskega peska, ostanek se bo zveličal."
Isaya analia kuhusiana na Israeli, “Kama hesabu ya wana wa Israeli ingekuwa kama mchanga wa bahari, itakuwa ni masalia ambao wataokolewa.
28 Kajti besedo je dokončeval in skrajševal v pravici, da bo besedo skrajšano storil Gospod na zemlji."
Kwa kuwa Bwana atalichukua neno lake juu ya nchi, mapema na kwa utimilifu.
29 In kakor je najprej povedal Izaija: "Ko bi Gospod: Sabaot, ne bil pustil nam semena, kakor Sodoma bili bi postali in Gomori podobni.")
Na kama jinsi Isaya alivyosema awali, “Kama Bwana wa majeshi hakutuachia nyuma uzao kwa ajili yetu, tungekuwa kama Sodoma, na tungefanywa kama Gomora.
30 Kaj torej porečemo? da so pogani, kteri niso iskali pravice, dobili pravico, ali pravico, ktera je iz vere;
Tutasema nini basi? kwamba watu wa Mataifa ambao walikuwa hawatafuti haki, walipata haki, haki kwa imani.
31 A Izrael iskajoč postavo pravice na postavo pravice ni zadel?
Lakini Israeli, ambaye alitafuta sheria ya haki, hakuifikia.
32 Za voljo česa? ker ni iz vere, nego kakor iz del pravice; kajti spotaknili so se ob kamen spotike,
Kwanini si hivyo? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani, bali kwa matendo. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa,
33 Kakor je pisano: Glej, polagam v Sionu kamen spotike in skalo pohujšanja; in kdorkoli veruje v njega, osramotil se ne bo.
kama ilivyo kwisha andikwa, “Tazama, nimelaza jiwe la kujikwaa katika Sayuni na mwamba wa kukosa. Yeye ambaye huamini katika hili hataaibika.”