< 2 Janez 1 >

1 Starejšina gospé izvoljeni in otrokom njenim, katere jaz ljubim v resnici, (in ne jaz sam, nego tudi vsi, ki so spoznali resnico),
Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
2 Po resnici, katera ostaja v nas, in z nami bode vekomaj; (aiōn g165)
kwa sababu ukweli unakaa nasi milele. (aiōn g165)
3 Z vami bode milost, usmiljenje, mir od Boga očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa, sina očetovega, v resnici in ljubezni.
Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
4 Veselil sem se močno, ker sem našel izmed otrok tvojih, ki hodijo v resnici, kakor smo zapoved dobili od očeta.
Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
5 In sedaj te prosim, pospá, ne da bi ti pisal novo zapoved, nego katero smo imeli od začetka, da se ljubimo med seboj.
Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
6 In to je ljubezen, da živimo po zapovedih njegovih. To je zapoved, kakor ste slišali od začetka, da v njej živite;
Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
7 Ker mnogi sleparji prišli so na svet, kateri ne spoznavajo Jezusa Kristusa, da je prišel v mesu. Ta je slepar in protikrist.
Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
8 Pazite, da ne izgubimo, kar smo pridelali, nego dobimo polno plačilo.
Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
9 Vsak, kdor prestopa in ne ostaja v uku Kristusovem, nima Boga; kdor ostaja v uku Kristusovem, ta ima očeta in sina.
Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
10 Če kdo pride k vam, in ne prinese tega uka, ne sprejemajte ga v hišo, in ne pozdravljajte ga;
Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
11 Kajti kdor ga pozdravlja, udeležuje se hudobnih del njegovih.
Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
12 Mnogo sem imel vam pisati, a nisem hotel s papirjem in črnilom; ali upam priti k vam, in iz ust do ust govoriti, da bode veselje vaše popolno.
Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
13 Pozdravljajo te otroci sestre tvoje izvoljene. Amen.
Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.

< 2 Janez 1 >