< Marko 16 >

1 Ko je šabat minil, so Marija Magdalena in Marija, Jakobova mati in Salóma kupile prijetne dišave, da bi lahko prišle ter ga pomazilile.
Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
2 In zelo zgodaj zjutraj, prvega dne v tednu, so ob sončnem vzhodu prišle k mavzoleju.
Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini.
3 In med seboj so govorile: »Kdo nam bo odvalil kamen proč izpred vrat mavzoleja?«
Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”
4 Ko pa so pogledale, so videle, da je bil kamen odvaljen proč, kajti bil je zelo velik.
Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
5 In vstopajoč v mavzolej, so zagledale mladeniča, ki je sedel na desni strani, oblečenega v dolgo belo obleko; in bile so zgrožene.
Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
6 On pa jim reče: »Ne bodite zgrožene. Ve iščete Jezusa Nazarečana, ki je bil križan. Obujen je, ni ga tukaj. Poglejte prostor, kamor so ga položili.
Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
7 Toda pojdite svojo pot, povejte njegovim učencem in Petru, da gre pred vami v Galilejo; tam ga boste videli, kakor vam je rekel.«
Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’”
8 In hitro so odšle ven in pobegnile od mavzoleja, kajti trepetale so in bile osuple niti niso ničesar povedale nobenemu človeku, kajti bile so prestrašene.
Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.
9 (note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Ko je torej Jezus zgodaj prvega dne v tednu vstal, se je najprej prikazal Mariji Magdaleni, iz katere je izgnal sedem hudičev.
(note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
10 In odšla je ter povedala tem, ki so bili z njim, ki so žalovali in jokali.
Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
11 In ko so slišali, da je bil živ in da ga je videla, niso verovali.
Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
12 Nató se je v drugi obliki prikazal dvema izmed njih, ki sta hodila in šla na deželo.
Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
13 In odšla sta ter to povedala preostalim. Niti njima niso verovali.
Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
14 Potem se je prikazal enajsterim, ko so sedeli pri obedu in jih oštel zaradi njihove nevere in trdote srca, ker niso verjeli tem, ki so ga videli potem, ko je bil obujen.
Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
15 In rekel jim je: »Pojdite po vsem svetu in oznanite evangelij vsakemu ustvarjenemu bitju.
Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Kdor veruje in je krščen, bo rešen; toda kdor ne veruje, bo obsojen.
Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
17 In ta znamenja bodo spremljala tiste, ki verujejo: ›V mojem imenu bodo izganjali hudiče, govorili bodo z novimi jeziki,
Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
18 dvigali bodo kače in če popijejo kakršnokoli smrtonosno stvar, jim ta ne bo škodila; polagali bodo roke na bolne in ti bodo ozdraveli.‹«
watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
19 Tako je bil potem, ko jim je Gospod govoril, sprejet gor v nebo in je sédel na Božjo desnico.
Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
20 Oni pa so šli naprej ter povsod oznanjali in Gospod je delal z njimi in besedo potrjeval s spremljajočimi znamenji. Amen.
Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]

< Marko 16 >