< Marko 15 >
1 In takoj zjutraj so imeli visoki duhovniki posvet s starešinami in pisarji ter celotnim vélikim zborom in zvezali Jezusa in ga odvedli proč ter ga izročili Pilatu.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 In Pilat ga je vprašal: »Ali si ti Kralj Judov?« In odgovoril je ter mu rekel: »Ti praviš to.«
Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 In visoki duhovniki so ga obtožili mnogih stvari. Toda nič ni odgovoril.
Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 In Pilat ga je ponovno vprašal, rekoč: »Nič ne odgovarjaš? Glej, koliko stvari pričujejo zoper tebe.«
Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 Vendar Jezus še vedno ni nič odgovoril, tako da se je Pilat čudil.
Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Torej na ta praznik jim je izpustil enega jetnika, kateregakoli so želeli.
Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 Tam pa je bil nekdo, imenovan Baraba, ki je ležal zvezan s temi, ki so z njim storili upor in ki je v uporu zagrešil umor.
Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 In množica je na glas kričala in začela zahtevati, da stori, kakor jim je vedno storil.
Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 Toda Pilat jim je odgovoril, rekoč: »Hočete, da vam izpustim Kralja Judov?«
Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
10 Kajti vedel je, da so mu ga visoki duhovniki izročili iz zavisti.
Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 Toda visoki duhovniki so napeljali množico, da naj jim raje izpusti Baraba.
Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 Pilat pa je odgovoril in jim ponovno rekel: »Kaj potem hočete, da naj storim tistemu, ki ga imenujete Kralj Judov?«
Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 In ponovno so zavpili: »Križaj ga.«
Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
14 Potem jim je Pilat rekel: »Zakaj, kakšno zlo je storil?« Oni pa so še bolj silno vpili: »Križaj ga.«
Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 In tako jim je Pilat, voljan ustreči množici, izpustil Baraba in ko je prebičal Jezusa, ga je izročil, da bi bil križan.
Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 In vojaki so ga odvedli proč v dvorano, imenovano Praetorium in sklicali vso četo.
Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 In oblekli so ga s škrlatom in spletli krono iz trnja ter jo nadeli na njegovo glavo
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18 in ga začeli pozdravljati: »Pozdravljen, Kralj Judov!«
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 In s trstom so ga udarjali po glavi in pljuvali nanj in ko so upogibali svoja kolena, so ga oboževali.
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 In ko so ga zasmehovali, so z njega sneli škrlat in nanj nadeli njegova lastna oblačila ter ga odvedli ven, da ga križajo.
Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 Prisilili pa so nekega Simona Cirenca, Aleksandrovega in Rufovega očeta, ki je šel mimo in prihajal iz dežele, da nese njegov križ.
Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 In privedli so ga na kraj Golgota, kar je prevedeno: ›Kraj lobanje.‹
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 In dali so mu za piti vina, pomešanega z miro, toda ni ga sprejel.
Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 In ko so ga križali, so razdelili njegove obleke in zanje metali žreb, kaj naj bi vsak mož vzel.
Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 In bila je tretja ura, oni pa so ga križali.
Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 In napis njegove obtožbe je bil napisan nad njim: KRALJ JUDOV.
Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 In z njim so križali dva tatova; enega na njegovi desni roki, drugega pa na njegovi levi.
Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
28 In pismo je bilo izpolnjeno, ki pravi: »In bil je prištet skupaj s prestopniki.«
Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Tisti pa, ki so hodili mimo, so se mu posmehovali in zmajevali s svojimi glavami ter govorili: »Ah, ti, ki uničiš tempelj in ga v treh dneh zgradiš,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 reši samega sebe in pridi dol s križa.«
basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 Podobno so ga zasmehovali tudi visoki duhovniki in s pisarji med seboj govorili: »Druge je rešil; sebe ne more rešiti.
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 Naj se Kristus, Izraelov Kralj, torej spusti s križa, da bomo lahko videli in verovali.« Ta dva, ki sta bila križana z njim, pa sta ga zasramovala.
Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 In ko je prišla šesta ura, je bila tema čez vso deželo do devete ure.
Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 Ob deveti uri pa je Jezus z močnim glasom zavpil, rekoč: »Eloí, Eloí, lemá sabahtáni?« kar je prevedeno: »Moj Bog, moj Bog, zakaj si me zapustil?«
Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 Nekateri izmed teh, ki so stali poleg, pa so, ko so to slišali, rekli: »Glejte, Elija kliče.«
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
36 In nekdo je stekel ter celotno gobo napojil s kisom in jo nataknil na trst in mu dal piti, rekoč: »Pustite pri miru; poglejmo, ali bo prišel Elija, da ga sname dol.«
Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 In Jezus je z močnim glasom zavpil in izročil duha.
Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 In tempeljsko zagrinjalo se je raztrgalo na dvoje od vrha do tal.
Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 Ko je stotnik, ki je stal poleg, njemu nasproti, videl, da je tako zavpil in izročil duha, je rekel: »Resnično, ta človek je bil Božji Sin.«
Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 Tam so bile tudi ženske, ki so gledale od daleč; med katerimi je bila Marija Magdalena in Marija, mater Jakoba mlajšega in od Jozéja in Salóma
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 (ki so mu, ko je bil v Galileji, tudi sledile in mu služile) in mnoge druge ženske, ki so z njim prišle gor v Jeruzalem.
Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
42 In sedaj, ko je prišel večer, ker je bila priprava, to je dan pred šabat,
Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
43 je Jožef iz Arimateje, častitljiv svetovalec, ki je prav tako pričakoval Božje kraljestvo, prišel in pogumno stopil k Pilatu ter prosil za Jezusovo telo.
Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
44 In Pilat se je začudil, da je bil že mrtev; in ko je k sebi poklical stotnika, ga je vprašal ali je bil že nekaj časa mrtev.
Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
45 In ko je od stotnika to izvedel, je telo poklonil Jožefu.
Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 In ta je kupil tanko laneno platno in ga snel ter zavil v laneno platno in ga položil v mavzolej, ki je bil izklesan iz skale in k vratom mavzoleja zavalil kamen.
Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 Marija Magdalena in Marija, Jozéjeva mati, pa sta opazovali, kam je bil položen.
Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.