< Псалтирь 105 >
1 Исповедайтеся Господеви и призывайте имя Его, возвестите во языцех дела Его:
Mshukuruni Yahwe, liitieni jina lake; myafanye matendo yake yajulikane kati ya mataifa.
2 воспойте Ему и пойте Ему, поведите вся чудеса Его.
Mwimbieni yeye, mwimbieni sifa yeye; semeni matendo yake yote ya ajau.
3 Хвалитеся о имени святем Его: да возвеселится сердце ищущих Господа:
Mjivune katika utakatifu wa jina lake; moyo wao wamtafutao Yahwe ufurahi.
4 взыщите Господа и утвердитеся, взыщите лица Его выну.
Mtafuteni Yahwe na nguvu zake; utafuteni uwepo wake siku zote.
5 Помяните чудеса Его, яже сотвори, чудеса Его и судбы уст Его,
Kumbukeni mambo ya ajabu aliyoyatenda,
6 семя Авраамле раби Его, сынове Иаковли избраннии Его.
miujiza yake na amri zitokazo kinywani mwake, enyi kizazi cha Ibrahimu mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wachaguliwa wake.
7 Той Господь Бог наш: по всей земли судбы Его.
Yeye ni Yahwe, Mungu wetu. Amri zake ziko juu ya nchi yote.
8 Помяну в век завет Свой, слово, еже заповеда в тысящы родов,
Naye hulikumbuka agano lake milele, neno alilo amuru kwa ajili ya vizazi elfu.
9 еже завеща Аврааму, и клятву Свою Исааку:
Hulikumbuka agano alilolifanya na Ibrahimu na kiapo alicho mwapia Isaka.
10 и постави ю Иакову в повеление и Израилю в завет вечен,
Hiki ndicho alicho mthibitishia Yakobo kama agano na kama agano la milele kwa Israeli.
11 глаголя: тебе дам землю Ханааню, уже достояния вашего.
Alisema, “Nitakupa wewe ardhi ya Kanaani kama sehemu yako ya urithi.”
12 Внегда быти им малым числом, малейшым и пришелцем в ней,
Alisema hili wakati tu walipokuwa wachache katika hesabu, yaani wachahe sana, nao walikuwa wageni katika nchi.
13 и преидоша от языка в язык и от царствия в люди ины:
Walienda taifa hadi taifa na kutoka ufalme moja kwenda mwingine.
14 не остави человека обидети их и обличи о них цари:
Hakuruhusu yeyote kuwaonea; aliwakemea wafalme kwa ajili yao.
15 не прикасайтеся помазанным Моим, и во пророцех Моих не лукавнуйте.
Alisema, “Msiwaguze wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
16 И призва глад на землю: всяко утверждение хлебное сотры.
Aliita njaa katika nchi; akaondoa upatikanaji wa mkate wote.
17 Посла пред ними человека: в раба продан бысть Иосиф.
Akatuma mtu mbele yao; Yusufu aliuzwa kama mtumishi.
18 Смириша во оковах нозе его, железо пройде душа его,
Miguu yake ilifungwa kwa pingu; alivishwa mnyororo wa chuma shingoni mwake,
19 дондеже прииде слово Его: слово Господне разжже его.
mpaka wakati wa maneno yake ulipotimia, nalo neno la Yahwe lilimjaribu.
20 Посла царь и разреши его: князь людий, и остави его.
Mfalme alituma watumishi kumfungua; mtawala wa watu alimuweka huru.
21 Постави его господина дому своему и князя всему стяжанию своему,
Alimuweka kuwa msimamizi wa nyumba yake kama mtawala wa mali zake zote
22 наказати князи его яко себе и старцы его умудрити.
kuwaelekeza wakuu kama alivyopenda na kuwafundisha viongozi wake hekima.
23 И вниде Израиль во Египет, и Иаков пришелствова в землю Хамову.
Kisha Israeli iliingia Misri, na Yakobo aliishi kwa muda katika nchi ya Hamu.
24 И возрасти люди Своя зело и укрепи я паче врагов их.
Yahwe aliwajalia watu wake wazae sana, na aliwafanya wenye nguvu kuliko adui zao.
25 Преврати сердце их возненавидети люди Его, лесть сотворити в рабех Его.
Alisababisha adui zao wawachukie watu wake, na kuwatendea visivyo watumishi wake.
26 Посла Моисеа раба Своего, Аарона, егоже избра себе:
Alimtuma Musa, mtumishi wake, na Haruni, ambaye alikwisha mchagua.
27 положи в них словеса знамений Своих и чудес Своих в земли Хамове.
Walifanya ishara zake kati ya Wamisri na maajabu yake katika ya nchi ya Hamu.
28 Посла тму и помрачи, яко преогорчиша словеса Его.
Alituma giza na likaifanya nchi hiyo kuwa giza, lakini watu wake hawakutii amri zake.
29 Преложи воды их в кровь и измори рыбы их.
Aligeuza maji kuwa damu na aliua samaki wao.
30 Воскипе земля их жабами в сокровищницах царей их.
Nchi yao ilijaa vyura, hata katika vyumba vya watawala wao.
31 Рече, и приидоша песия мухи и скнипы во вся пределы их.
Alisema, na makundi ya inzi na chawa wakaja mjini mwote.
32 Положи дожди их грады, огнь попаляющь в земли их:
Aliigeuza mvua yao kuwa mvua ya mawe, pamoja na miali ya moto juu ya ardhi yao.
33 и порази винограды их и смоквы их, и сотры всякое древо предел их.
Aliiharibu mizabibu yao na mitini yao; akaivunja miti ya mji wao.
34 Рече, и приидоша прузи и гусеницы, имже не бе числа,
Alisema, na nzige wakaja, nzige wengi sana.
35 и снедоша всяку траву в земли их, и поядоша всяк плод земли их.
Nzige walikula mboga zao zote za majani katika nchi yao. Walikula mazao yote ardhini.
36 И порази всякаго первенца в земли их, начаток всякаго труда их:
Aliua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao, malimbuko ya nguvu zao.
37 и изведе я с сребром и златом: и не бе в коленех их боляй.
Aliwatoa nje Waisraeli wakiwa na fedha na dhahabu; hakuna mmoja wa kabila lake aliyejikwaa njiani.
38 Возвеселися Египет во исхождении их: яко нападе страх их на ня.
Misri ilifurahi walipoondoka, maana Wamisri waliwaogopa.
39 Распростре облак в покров им, и огнь, еже просветити им нощию.
Alitandaza wingu liwafunike na alifanya moto uwaangazie wakati wa usiku.
40 Просиша, и приидоша крастели, и хлеба небеснаго насыти я:
Waisraeli waliomba chakula, naye aliwaletea kware na aliwatosheleza kwa mkate kutoka mbiguni.
41 разверзе камень, и потекоша воды, потекоша в безводных реки:
Aliugawa mwamba, maji yalimwagika kutoka humo; yalitiririka katika jangwa kama mto.
42 яко помяну слово святое Свое, еже ко Аврааму рабу Своему.
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu aliyoifanya kwa Ibrahimu mtumishi wake.
43 И изведе люди Своя в радости и избранныя Своя в веселии.
Aliwaongoza watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za ushindi.
44 И даде им страны язык, и труды людий наследоваша:
Aliwapa nchi za mataifa; walichukua milki ya mali za watu
45 яко да сохранят оправдания Его и закона Его взыщут.
ili waweze kushika amri zake na kutii sheria zake. Msifuni Yahwe.