< Псалтирь 109 >
1 Боже, хвалы моея не премолчи:
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 яко уста грешнича и уста льстиваго на мя отверзошася, глаголаша на мя языком льстивым,
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 и словесы ненавистными обыдоша мя, и брашася со мною туне.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 Вместо еже любити мя, оболгаху мя, аз же моляхся:
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 и положиша на мя злая за благая, и ненависть за возлюбление мое.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Постави на него грешника, и диавол да станет одесную его:
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 внегда судитися ему, да изыдет осужден, и молитва его да будет в грех.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Да будут дние его мали, и епископство его да приимет ин:
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 да будут сынове его сири, и жена его вдова:
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 движущеся да преселятся сынове его и воспросят, да изгнани будут из домов своих.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Да взыщет заимодавец вся, елика суть его: и да восхитят чуждии труды его.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 Да не будет ему заступника, ниже да будет ущедряяй сироты его:
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 да будут чада его в погубление, в роде единем да потребится имя его.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 Да воспомянется беззаконие отец его пред Господем, и грех матере его да не очистится:
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 да будут пред Господем выну, и да потребится от земли память их:
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 занеже не помяну сотворити милость, и погна человека нища и убога, и умилена сердцем умертвити.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 И возлюби клятву, и приидет ему: и не восхоте благословения, и удалится от него.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 И облечеся в клятву яко в ризу, и вниде яко вода во утробу его и яко елей в кости его:
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 да будет ему яко риза, в нюже облачится, и яко пояс, имже выну опоясуется.
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Сие дело оболгающих мя у Господа и глаголющих лукавая на душу мою.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 И Ты, Господи, Господи, сотвори со мною имене ради Твоего, яко блага милость Твоя:
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 избави мя, яко нищь и убог есмь аз, и сердце мое смятеся внутрь мене.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Яко сень, внегда уклонитися ей, отяхся: стрясохся яко прузи.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 Колена моя изнемогоста от поста, и плоть моя изменися елеа ради.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 И аз бых поношение им: видеша мя, покиваша главами своими.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Помози ми, Господи Боже мой, и спаси мя по милости Твоей:
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 и да разумеют, яко рука Твоя сия, и Ты, Господи, сотворил еси ю.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Прокленут тии, и Ты благословиши: востающии на мя да постыдятся, раб же Твой возвеселится.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Да облекутся оболгающии мя в срамоту и одеждутся яко одеждою студом своим.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 Исповемся Господеви зело усты моими и посреде многих восхвалю Его:
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 яко преста одесную убогаго, еже спасти от гонящих душу мою.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.