< Исход 12 >

1 Рече же Господь к Моисею и Аарону в земли Египетстей, глаголя:
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 месяц сей вам начало месяцей, первый будет вам в месяцех лета:
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 рцы ко всему сонму сынов Израилевых, глаголя: в десятый месяца сего да возмет кийждо овча по домом отечеств, кийждо овча по дому:
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 аще же мало их есть в дому, яко не доволным быти на овча, да возмет с собою соседа ближняго своего по числу душ: кийждо доволное себе сочтет на овча:
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 овча совершенно, мужеск пол, непорочно и единолетно будет вам, от агнец и от козлищ приимете:
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 и будет вам соблюдено даже до четвертагонадесять дне месяца сего: и заколют то все множество собора сынов Израилевых к вечеру,
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 и приимут от крове и помажут на обою подвою и на прагах в домех, в нихже снедят тое,
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 и снедят мяса в нощи той печена огнем и опресноки с горьким зелием снедят:
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 не снесте от них сурово, ниже варено в воде, но печеное огнем, главу с ногами и со утробою:
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 не оставите от него до утрия и кости не сокрушите от него, останки же от него до утра огнем сожжете:
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 сице же снесте е: чресла ваша препоясана, и сапози ваши на ногах ваших, и жезлы ваши в руках ваших, и снесте е со тщанием: Пасха есть Господня:
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 и пройду землю Египетскую сея нощи, и убию всякаго первенца в земли Египетстей, от человека до скота, и во всех бозех Египетских сотворю отмщение: Аз Господь:
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 и будет кровь вам в знамение на домех, в нихже вы будете тамо, и узрю кровь и покрыю вы, и не будет в вас язвы, еже погибнути, егда поражу землю Египетскую:
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 и будет вам день сей в память, и празднуйте той праздник Господу во вся роды вашя: законно вечно празднуйте его:
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 седмь дний опресноки ядите, от перваго же дне измите квас из домов ваших: всяк, иже снесть кисло, погибнет душа та от Израиля, от дне перваго даже до дне седмаго:
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 и первый день наречется свят, и седмый день нарочит свят да будет вам: всякаго дела работна да не сотворите в них, разве елика (снести) сотворятся всякой души, сия точию да сотворятся вам:
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 и сохраните заповедь сию: в сей бо день изведу силу вашу от земли Египетския: и сотворите день сей в роды вашя, законно вечно:
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 начинающе в четвертыйнадесять день перваго месяца, с вечера да снесте опресноки, до двадесять перваго дне месяца, до вечера:
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
19 седмь дний квас да не явится в домех ваших: всяк, иже аще снесть квасно, погубится душа та от сонма сынов Израилевых и в пришелцех и в жителех тоя земли:
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 всякаго кваснаго да не ясте, во всех же домех ваших да ясте опресноки.
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Созва же Моисей вся старцы сынов Израилевых и рече им: шедше поимите себе овча по сродством вашым и пожрите пасху:
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 возмите же кисть иссопа, и омочивше в кровь, яже близ дверий, помажите праги, и на обою подвою, от крове, яже есть близ дверий: вы же да не изыдете кийждо из дверий дому своего до заутрия:
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 и мимо пройдет Господь избити Египтяны, и узрит кровь на празе и на обою подвою, и минет Господь двери, и не попустит погубляющему внити в домы вашя убивати:
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 и сохраните слово сие законно себе и сыном вашым до века:
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 аще же внидете в землю, юже даст Господь вам, якоже глагола, сохраните служение сие,
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 и будет егда возглаголют вам сынове ваши: что есть служение сие?
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 И рцыте им: жертва пасха сия Господу, Иже покры домы сынов Израилевых во Египте, егда поби Египтяны, домы же нашя избави. И преклоншеся людие поклонишася.
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 И отшедше сотвориша сынове Израилевы, якоже заповеда Господь Моисею и Аарону, тако сотвориша.
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 Бысть же в полунощи, и Господь порази всякаго первенца в земли Египетстей, от первенца фараонова седящаго на престоле, до первенца пленницы, яже в рове, и до первенца всякаго скотска.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 Воста же фараон нощию, и вси раби его, и вси Египтяне, и бысть вопль велик по всей земли Египетстей, ибо не бысть дом, в немже не бе мертвеца.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 И призва фараон Моисеа и Аарона в нощи и рече им: востаните и отидите от людий моих, и вы, и сынове Израилевы: идите и послужите Господу Богу вашему, якоже глаголете:
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 и овцы и говяда вашя поимше идите, благословите же и мене.
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 И нуждаху Египтяне людий со тщанием изринути их от земли: рекоша бо, яко вси мы измрем.
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 Взяша же людие муку свою прежде вскисения теста своего, и ввязавше в ризы, (возложиша) на рамы своя.
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 Сынове же Израилевы сотвориша, якоже заповеда им Моисей: и испросиша от Египтян сосуды сребряны и златы, и ризы:
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 и даде Господь благодать людем Своим пред Египтяны: и даша им, и обраша Египтян.
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 Воздвигошася же сынове Израилевы от Рамессы в Сокхоф до шести сот тысящ пеших мужей, кроме домочадства:
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 и пришелцы мнози изыдоша с ними, и овцы, и волы, и скоти мнози зело.
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 И испекоша тесто, еже изнесоша из Египта, опресноки не кислы, не вскисоша бо: ибо изгнаша их Египтяне, и не возмогоша помедлити, ниже брашна сотвориша себе на путь.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 Обитания же сынов Израилевых, иже обиташа в земли Египетстей и в земли Ханаани сии и отцы их, лет четыреста тридесять.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 И бысть по четырех стех и тридесяти летех, изыде вся сила Господня от земли Египетския в нощи.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 Стражба есть Господу, еже извести их от земли Египетския: оная нощь самая стражба Господу, яко всем сыном Израилевым быти в роды их.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 И рече Господь к Моисею и Аарону: сей закон Пасхи: всяк иноплеменник да не яст от нея,
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44 и всякаго раба или купленаго обрежеши его, и тогда да яст от нея:
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 пришлец или наемник да не яст от нея:
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 в дому единем да снестся: не оставите от мяс на утрие, и не изнесите мяс вон из дому, и кости не сокрушите от него:
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 весь сонм сынов Израилевых сотворит сие:
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 аще же кто приидет пришлец к вам сотворити Пасху Господню, обрежеши его всяк мужеский пол, и тогда приступит сотворити ю, и будет аки житель земли тоя: всяк же необрезаный да не яст от нея:
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 закон един да будет тоя земли жителю и пришелцу пришедшему в вас.
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 И сотвориша сынове Израилевы, якоже заповеда Господь Моисею и Аарону, тако сотвориша.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 И бысть в день он, изведе Господь сыны Израилевы от земли Египетския с силою их.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

< Исход 12 >