< Zaharija 11 >

1 Otvori, Livane, vrata svoja, i oganj neka proždre kedre tvoje.
Fungua milango yako, ee Lebanoni, ili moto uteketeze mierezi yako!
2 Ridaj, jelo, jer pade kedar, jer krasnici propadoše; ridajte, hrastovi Vasanski, jer se posijeèe šuma ograðena.
Piga yowe, ee mti wa msunobari, kwa kuwa mwerezi umeanguka; miti ya fahari imeharibiwa! Piga yowe, enyi mialoni ya Bashani, msitu mnene umefyekwa!
3 Stoji jauk pastira, jer se zatr slava njihova; stoji rika lavova, jer se opustoši ponos Jordanski.
Sikiliza yowe la wachungaji; malisho yao manono yameangamizwa! Sikia ngurumo za simba; kichaka kilichostawi sana cha Yordani kimeharibiwa!
4 Ovako veli Gospod Bog moj: pasi ovce klanice,
Hili ndilo asemalo Bwana Mungu wangu: “Lilishe kundi lililokusudiwa kuchinjwa.
5 Koje ubijaju oni koji ih drže, niti ih ko krivi, i koji ih prodaju govore: blagosloven da je Gospod, obogatih se; i koji ih pasu, nijedan ih ne žali.
Wanunuzi wake huwachinja na kuondoka pasipo kuadhibiwa. Wale wanaowauza husema, ‘Bwana asifiwe, mimi ni tajiri!’ Wachungaji wao wenyewe hawawahurumii.
6 Zato neæu više žaliti stanovnika zemaljskih, govori Gospod, nego æu evo predati jednoga drugome u ruke i u ruke caru njihovu, i oni æe potrti zemlju a ja je neæu izbaviti iz ruku njihovijeh.
Kwa kuwa sitawahurumia tena watu wa nchi,” asema Bwana. “Nitawakabidhi kila mtu mkononi mwa jirani yake na mfalme wake. Wataitenda jeuri nchi, nami sitawaokoa kutoka mikononi mwao.”
7 I pasoh ovce klanice, nevoljne od stada, i uzev dva štapa nazvah jedan blagost, a drugi nazvah sveza, i pasoh stado.
Kwa hiyo nikalilisha kundi lililotiwa alama kwa kuchinjwa, hasa kundi lililoonewa sana. Kisha nikachukua fimbo mbili, moja nikaiita Fadhili na nyingine Umoja, nami nikalilisha kundi.
8 I pogubih tri pastira za mjesec dana, jer se duša moja ljuæaše na njih, i duša njihova mržaše na me.
Katika mwezi mmoja nikawaondoa wachungaji watatu. Kundi la kondoo likanichukia, nami nikachoshwa nao,
9 I rekoh: neæu vas više pasti; koja pogine neka pogine, i koja propadne neka propadne, i koje ostanu neka jedu meso jedna drugoj.
nikasema, “Sitakuwa mchungaji wenu. Waache wanaokufa wafe na wanaoangamia waangamie. Wale waliobakia kila mmoja na ale nyama ya mwenzake.”
10 I uzeh svoj štap, blagost, i slomih ga da ukinem zavjet svoj koji uèinih sa svijem narodima.
Kisha nikachukua fimbo yangu inayoitwa Fadhili nikaivunja, kutangua Agano nililofanya na mataifa yote.
11 I ukide se onoga dana, i nevoljni od stada, koji gledahu na me, poznaše doista da bješe rijeè Gospodnja.
Likatanguka siku hiyo, kwa hiyo wale waliodhurika katika kundi, waliokuwa wakiniangalia wakajua kuwa hilo lilikuwa neno la Bwana.
12 I rekoh im: ako vam je drago, dajte mi moju platu; ako li nije, nemojte; i izmjeriše mi platu, trideset srebrnika.
Nikawaambia, “Mkiona kuwa ni vyema, nipeni ujira wangu, la sivyo, basi msinipe.” Kwa hiyo wakanilipa vipande thelathini vya fedha.
13 I reèe mi Gospod: baci lonèaru tu èasnu cijenu kojom me precijeniše. I uzev trideset srebrnika bacih ih u dom Gospodnji lonèaru.
Naye Bwana akaniambia, “Mtupie mfinyanzi,” hiyo bei nzuri waliyonithaminia! Kwa hiyo nikachukua hivyo vipande thelathini vya fedha na kumtupia huyo mfinyanzi katika nyumba ya Bwana.
14 Potom slomih drugi štap svoj, svezu, da ukinem bratstvo izmeðu Jude i Izrailja.
Kisha nikaivunja fimbo yangu ya pili iitwayo Umoja, kuvunja undugu kati ya Yuda na Israeli!
15 I Gospod mi reèe: uzmi jošte opravu bezumna pastira.
Kisha Bwana akaniambia, “Vitwae tena vifaa vya mchungaji mpumbavu.
16 Jer evo ja æu podignuti pastira u zemlji, koji neæe obilaziti one koja gine, neæe tražiti nejake, niti æe lijeèiti ranjene, niti æe nositi sustale, nego æe jesti meso od pretilijeh, i papke æe im kidati.
Kwa maana ninakwenda kumwinua mchungaji juu ya nchi ambaye hatamjali aliyepotea, wala kuwatafuta wale wachanga au kuwaponya waliojeruhiwa, wala kuwalisha wenye afya, lakini atakula nyama ya kondoo wanono na kuzirarua kwato zao.
17 Teško pastiru nikakom, koji ostavlja stado! Maè mu je nad mišicom i nad desnijem okom; mišica æe mu usahnuti i desno æe mu oko potamnjeti.
“Ole wa mchungaji asiyefaa, anayeliacha kundi! Upanga na uupige mkono wake na jicho lake la kuume! Mkono wake na unyauke kabisa, jicho lake la kuume lipofuke kabisa!”

< Zaharija 11 >