< 1 yOhanaH 4 >
1 hE priyatamAH, yUyaM sarvvESvAtmasu na vizvasita kintu tE IzvarAt jAtA na vEtyAtmanaH parIkSadhvaM yatO bahavO mRSAbhaviSyadvAdinO jaganmadhyam AgatavantaH|
Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni.
2 IzvarIyO ya AtmA sa yuSmAbhiranEna paricIyatAM, yIzuH khrISTO narAvatArO bhUtvAgata Etad yEna kEnacid AtmanA svIkriyatE sa IzvarIyaH|
Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu.
3 kintu yIzuH khrISTO narAvatArO bhUtvAgata Etad yEna kEnacid AtmanA nAggIkriyatE sa IzvarIyO nahi kintu khrISTArErAtmA, tEna cAgantavyamiti yuSmAbhiH zrutaM, sa cEdAnImapi jagati varttatE|
Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.
4 hE bAlakAH, yUyam IzvarAt jAtAstAn jitavantazca yataH saMsArAdhiSThAnakAriNO 'pi yuSmadadhiSThAnakArI mahAn|
Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
5 tE saMsArAt jAtAstatO hEtOH saMsArAd bhASantE saMsArazca tESAM vAkyAni gRhlAti|
Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza.
6 vayam IzvarAt jAtAH, IzvaraM yO jAnAti sO'smadvAkyAni gRhlAti yazcEzvarAt jAtO nahi sO'smadvAkyAni na gRhlAti; anEna vayaM satyAtmAnaM bhrAmakAtmAnanjca paricinumaH|
Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.
7 hE priyatamAH, vayaM parasparaM prEma karavAma, yataH prEma IzvarAt jAyatE, aparaM yaH kazcit prEma karOti sa IzvarAt jAta IzvaraM vEtti ca|
Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
8 yaH prEma na karOti sa IzvaraM na jAnAti yata IzvaraH prEmasvarUpaH|
Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo.
9 asmAsvIzvarasya prEmaitEna prAkAzata yat svaputrENAsmabhyaM jIvanadAnArtham IzvaraH svIyam advitIyaM putraM jaganmadhyaM prESitavAn|
Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake.
10 vayaM yad IzvarE prItavanta ityatra nahi kintu sa yadasmAsu prItavAn asmatpApAnAM prAyazcirttArthaM svaputraM prESitavAMzcEtyatra prEma santiSThatE|
Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.
11 hE priyatamAH, asmAsu yadIzvarENaitAdRzaM prEma kRtaM tarhi parasparaM prEma karttum asmAkamapyucitaM|
Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana.
12 IzvaraH kadAca kEnApi na dRSTaH yadyasmAbhiH parasparaM prEma kriyatE tarhIzvarO 'smanmadhyE tiSThati tasya prEma cAsmAsu sEtsyatE|
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
13 asmabhyaM tEna svakIyAtmanOM'zO datta ityanEna vayaM yat tasmin tiSThAmaH sa ca yad asmAsu tiSThatIti jAnImaH|
Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake.
14 pitA jagatrAtAraM putraM prESitavAn Etad vayaM dRSTvA pramANayAmaH|
Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu.
15 yIzurIzvarasya putra Etad yEnAggIkriyatE tasmin IzvarastiSThati sa cEzvarE tiSThati|
Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
16 asmAsvIzvarasya yat prEma varttatE tad vayaM jnjAtavantastasmin vizvAsitavantazca| IzvaraH prEmasvarUpaH prEmnI yastiSThati sa IzvarE tiSThati tasmiMzcEzvarastiSThati|
Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu. Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake.
17 sa yAdRzO 'sti vayamapyEtasmin jagati tAdRzA bhavAma EtasmAd vicAradinE 'smAbhi ryA pratibhA labhyatE sAsmatsambandhIyasya prEmnaH siddhiH|
Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu.
18 prEmni bhIti rna varttatE kintu siddhaM prEma bhItiM nirAkarOti yatO bhItiH sayAtanAsti bhItO mAnavaH prEmni siddhO na jAtaH|
Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.
19 asmAsu sa prathamaM prItavAn iti kAraNAd vayaM tasmin prIyAmahE|
Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza.
20 IzvarE 'haM prIya ityuktvA yaH kazcit svabhrAtaraM dvESTi sO 'nRtavAdI| sa yaM dRSTavAn tasmin svabhrAtari yadi na prIyatE tarhi yam IzvaraM na dRSTavAn kathaM tasmin prEma karttuM zaknuyAt?
Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona?
21 ata IzvarE yaH prIyatE sa svIyabhrAtaryyapi prIyatAm iyam AjnjA tasmAd asmAbhi rlabdhA|
Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.