< prakAzitaM 3 >

1 aparaM sArddisthasamitE rdUtaM pratIdaM likha, yO jana Izvarasya saptAtmanaH sapta tArAzca dhArayati sa Eva bhASatE, tava kriyA mama gOcarAH, tvaM jIvadAkhyO 'si tathApi mRtO 'si tadapi jAnAmi|
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika: “Haya ndiyo maneno ya aliye na zile Roho sabaza Mungu na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, kwamba una sifa ya kuwa hai, lakini umekufa.
2 prabuddhO bhava, avaziSTaM yadyat mRtakalpaM tadapi sabalIkuru yata Izvarasya sAkSAt tava karmmANi na siddhAnIti pramANaM mayA prAptaM|
Amka! Nawe uyaimarishe yale yaliyosalia na yaliyo karibu kufa, kwa maana sikuona kwamba kazi zako zimekamilika machoni pa Mungu wangu.
3 ataH kIdRzIM zikSAM labdhavAn zrutavAzcAsi tat smaran tAM pAlaya svamanaH parivarttaya ca| cEt prabuddhO na bhavEstarhyahaM stEna iva tava samIpam upasthAsyAmi kinjca kasmin daNPE upasthAsyAmi tanna jnjAsyasi|
Kumbuka basi yale uliyoyapokea na kuyasikia, yatii na ukatubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwizi wala hutajua saa nitakayokuja kwako.
4 tathApi yaiH svavAsAMsi na kalagkitAni tAdRzAH katipayalOkAH sArddinagarE 'pi tava vidyantE tE zubhraparicchadai rmama saggE gamanAgamanE kariSyanti yatastE yOgyAH|
“Lakini bado una watu wachache katika Sardi ambao hawajayachafua mavazi yao. Wao wataenda pamoja nami, wakiwa wamevaa mavazi meupe, kwa maana wanastahili.
5 yO janO jayati sa zubhraparicchadaM paridhApayiSyantE, ahanjca jIvanagranthAt tasya nAma nAntardhApayiSyAmi kintu matpituH sAkSAt tasya dUtAnAM sAkSAcca tasya nAma svIkariSyAmi|
Yeye ashindaye atavikwa vazi jeupe kama wao. Sitafuta jina lake kutoka kitabu cha uzima, bali nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu na mbele za malaika wake.
6 yasya zrOtraM vidyatE sa samitIH pratyucyamAnAm AtmanaH kathAM zRNOtu|
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
7 aparanjca philAdilphiyAsthasamitE rdUtaM pratIdaM likha, yaH pavitraH satyamayazcAsti dAyUdaH kunjjikAM dhArayati ca yEna mOcitE 'paraH kO'pi na ruNaddhi ruddhE cAparaH kO'pi na mOcayati sa Eva bhASatE|
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, yeye aliye na ufunguo wa Daudi. Anachokifungua hakuna awezaye kukifunga, wala anachokifunga hakuna awezaye kukifungua.
8 tava kriyA mama gOcarAH pazya tava samIpE 'haM muktaM dvAraM sthApitavAn tat kEnApi rOddhuM na zakyatE yatastavAlpaM balamAstE tathApi tvaM mama vAkyaM pAlitavAn mama nAmnO 'svIkAraM na kRtavAMzca|
Nayajua matendo yako. Tazama, nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, wala hakuna awezaye kuufunga. Ninajua kwamba una nguvu kidogo lakini umelishika neno langu wala hukulikana Jina langu.
9 pazya yihUdIyA na santO yE mRSAvAdinaH svAn yihUdIyAn vadanti tESAM zayatAnasamAjIyAnAM kAMzcid aham AnESyAmi pazya tE madAjnjAta Agatya tava caraNayOH praNaMsyanti tvanjca mama priyO 'sIti jnjAsyanti|
Nitawafanya wale wa sinagogi la Shetani, wale ambao husema kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali ni waongo, nitawafanya waje wapige magoti miguuni pako, na wakiri ya kwamba nimekupenda.
10 tvaM mama sahiSNutAsUcakaM vAkyaM rakSitavAnasi tatkAraNAt pRthivInivAsinAM parIkSArthaM kRtsnaM jagad yEnAgAmiparIkSAdinEnAkramiSyatE tasmAd ahamapi tvAM rakSiSyAmi|
Kwa kuwa umeshika amri yangu ya kuvumilia katika saburi, nitakulinda katika saa ya kujaribiwa inayokuja ulimwenguni pote, ili kuwajaribu wote wakaao duniani.
11 pazya mayA zIghram AgantavyaM tava yadasti tat dhAraya kO 'pi tava kirITaM nApaharatu|
“Ninakuja upesi. Shika sana ulicho nacho, ili mtu asije akaichukua taji yako.
12 yO janO jayati tamahaM madIyEzvarasya mandirE stambhaM kRtvA sthApayisyAmi sa puna rna nirgamiSyati| aparanjca tasmin madIyEzvarasya nAma madIyEzvarasya puryyA api nAma arthatO yA navInA yirUzAnam purI svargAt madIyEzvarasya samIpAd avarOkSyati tasyA nAma mamApi nUtanaM nAma lEkhiSyAmi|
Yeye ashindaye nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo kamwe. Nitaandika juu yake Jina la Mungu wangu na jina la mji mkubwa wa Mungu wangu, Yerusalemu mpya, ambao unashuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu. Nami pia nitaandika juu yake Jina langu jipya.
13 yasya zrOtraM vidyatE sa samitIH pratyucyamAnAm AtmanaH kathAM zRNOtu|
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
14 aparanjca lAyadikEyAsthasamitE rdUtaM pratIdaM likha, ya AmEn arthatO vizvAsyaH satyamayazca sAkSI, Izvarasya sRSTErAdizcAsti sa Eva bhASatE|
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye Amen, shahidi mwaminifu na wa kweli, mtawala wa uumbaji wote wa Mungu.
15 tava kriyA mama gOcarAH tvaM zItO nAsi taptO 'pi nAsIti jAnAmi|
Nayajua matendo yako, ya kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungelikuwa moja au lingine.
16 tava zItatvaM taptatvaM vA varaM bhavEt, zItO na bhUtvA taptO 'pi na bhUtvA tvamEvambhUtaH kadUSNO 'si tatkAraNAd ahaM svamukhAt tvAm udvamiSyAmi|
Hivyo kwa kuwa u vuguvugu, si baridi wala moto, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
17 ahaM dhanI samRddhazcAsmi mama kasyApyabhAvO na bhavatIti tvaM vadasi kintu tvamEva duHkhArttO durgatO daridrO 'ndhO nagnazcAsi tat tvayA nAvagamyatE|
Kwa maana unasema: ‘Mimi ni tajiri, nimejilimbikizia mali, wala sihitaji kitu chochote.’ Lakini hutambui ya kwamba wewe ni mnyonge, wa kuhurumiwa, maskini, kipofu, tena uliye uchi.
18 tvaM yad dhanI bhavEstadarthaM mattO vahnau tApitaM suvarNaM krINIhi nagnatvAt tava lajjA yanna prakAzEta tadarthaM paridhAnAya mattaH zubhravAsAMsi krINIhi yacca tava dRSTiH prasannA bhavEt tadarthaM cakSurlEpanAyAnjjanaM mattaH krINIhIti mama mantraNA|
Nakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, ili upate kuwa tajiri, na mavazi meupe ili uyavae upate kuficha aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka macho yako ili upate kuona.
19 yESvahaM prIyE tAn sarvvAn bhartsayAmi zAsmi ca, atastvam udyamaM vidhAya manaH parivarttaya|
“Wale niwapendao, ninawakemea na kuwaadibisha. Hivyo uwe na bidii ukatubu.
20 pazyAhaM dvAri tiSThan tad Ahanmi yadi kazcit mama ravaM zrutvA dvAraM mOcayati tarhyahaM tasya sannidhiM pravizya tEna sArddhaM bhOkSyE sO 'pi mayA sArddhaM bhOkSyatE|
Tazama! Nasimama mlangoni nabisha. Kama mtu yeyote akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami.
21 aparamahaM yathA jitavAn mama pitrA ca saha tasya siMhAsana upaviSTazcAsmi, tathA yO janO jayati tamahaM mayA sArddhaM matsiMhAsana upavEzayiSyAmi|
“Yeye ashindaye nitampa haki ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na nikaketi pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha enzi.
22 yasya zrOtraM vidyatE sa samitIH pratyucyamAnam AtmanaH kathAM zRNOtu|
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.”

< prakAzitaM 3 >