< 1 karinthinaH 12 >

1 hE bhrAtaraH, yUyaM yad AtmikAn dAyAn anavagatAstiSThatha tadahaM nAbhilaSAmi|
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2 pUrvvaM bhinnajAtIyA yUyaM yadvad vinItAstadvad avAkpratimAnAm anugAmina Adhbam iti jAnItha|
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3 iti hEtOrahaM yuSmabhyaM nivEdayAmi, IzvarasyAtmanA bhASamANaH kO'pi yIzuM zapta iti na vyAharati, punazca pavitrENAtmanA vinItaM vinAnyaH kO'pi yIzuM prabhuriti vyAharttuM na zaknOti|
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4 dAyA bahuvidhAH kintvEka AtmA
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5 paricaryyAzca bahuvidhAH kintvEkaH prabhuH|
Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
6 sAdhanAni bahuvidhAni kintu sarvvESu sarvvasAdhaka Izvara EkaH|
Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
7 Ekaikasmai tasyAtmanO darzanaM parahitArthaM dIyatE|
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 Ekasmai tEnAtmanA jnjAnavAkyaM dIyatE, anyasmai tEnaivAtmanAdiSTaM vidyAvAkyam,
Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
9 anyasmai tEnaivAtmanA vizvAsaH, anyasmai tEnaivAtmanA svAsthyadAnazaktiH,
Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
10 anyasmai duHsAdhyasAdhanazaktiranyasmai cEzvarIyAdEzaH, anyasmai cAtimAnuSikasyAdEzasya vicArasAmarthyam, anyasmai parabhASAbhASaNazaktiranyasmai ca bhASArthabhASaNasAmaryaM dIyatE|
Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
11 EkEnAdvitIyEnAtmanA yathAbhilASam Ekaikasmai janAyaikaikaM dAnaM vitaratA tAni sarvvANi sAdhyantE|
Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
12 dEha EkaH sannapi yadvad bahvaggayuktO bhavati, tasyaikasya vapuSO 'ggAnAM bahutvEna yadvad EkaM vapu rbhavati, tadvat khrISTaH|
Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
13 yatO hEtO ryihUdibhinnajAtIyadAsasvatantrA vayaM sarvvE majjanEnaikEnAtmanaikadEhIkRtAH sarvvE caikAtmabhuktA abhavAma|
Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 EkEnAggEna vapu rna bhavati kintu bahubhiH|
Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
15 tatra caraNaM yadi vadEt nAhaM hastastasmAt zarIrasya bhAgO nAsmIti tarhyanEna zarIrAt tasya viyOgO na bhavati|
Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
16 zrOtraM vA yadi vadEt nAhaM nayanaM tasmAt zarIrasyAMzO nAsmIti tarhyanEna zarIrAt tasya viyOgO na bhavati|
Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
17 kRtsnaM zarIraM yadi darzanEndriyaM bhavEt tarhi zravaNEndriyaM kutra sthAsyati? tat kRtsnaM yadi vA zravaNEndriyaM bhavEt tarhi ghraNEndriyaM kutra sthAsyati?
Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
18 kintvidAnIm IzvarENa yathAbhilaSitaM tathaivAggapratyaggAnAm EkaikaM zarIrE sthApitaM|
Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
19 tat kRtsnaM yadyEkAggarUpi bhavEt tarhi zarIrE kutra sthAsyati?
Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 tasmAd aggAni bahUni santi zarIraM tvEkamEva|
Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 ataEva tvayA mama prayOjanaM nAstIti vAcaM pANiM vadituM nayanaM na zaknOti, tathA yuvAbhyAM mama prayOjanaM nAstIti mUrddhA caraNau vadituM na zaknOtiH;
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
22 vastutastu vigrahasya yAnyaggAnyasmAbhi rdurbbalAni budhyantE tAnyEva saprayOjanAni santi|
Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
23 yAni ca zarIramadhyE'vamanyAni budhyatE tAnyasmAbhiradhikaM zObhyantE| yAni ca kudRzyAni tAni sudRzyatarANi kriyantE
Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
24 kintu yAni svayaM sudRzyAni tESAM zObhanam niSprayOjanaM|
wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
25 zarIramadhyE yad bhEdO na bhavEt kintu sarvvANyaggAni yad aikyabhAvEna sarvvESAM hitaM cintayanti tadartham IzvarENApradhAnam AdaraNIyaM kRtvA zarIraM viracitaM|
ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
26 tasmAd EkasyAggasya pIPAyAM jAtAyAM sarvvANyaggAni tEna saha pIPyantE, Ekasya samAdarE jAtE ca sarvvANi tEna saha saMhRSyanti|
Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 yUyanjca khrISTasya zarIraM, yuSmAkam Ekaikazca tasyaikaikam aggaM|
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
28 kEcit kEcit samitAvIzvarENa prathamataH prEritA dvitIyata IzvarIyAdEzavaktArastRtIyata upadESTArO niyuktAH, tataH paraM kEbhyO'pi citrakAryyasAdhanasAmarthyam anAmayakaraNazaktirupakRtau lOkazAsanE vA naipuNyaM nAnAbhASAbhASaNasAmarthyaM vA tEna vyatAri|
Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
29 sarvvE kiM prEritAH? sarvvE kim IzvarIyAdEzavaktAraH? sarvvE kim upadESTAraH? sarvvE kiM citrakAryyasAdhakAH?
Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
30 sarvvE kim anAmayakaraNazaktiyuktAH? sarvvE kiM parabhASAvAdinaH? sarvvE vA kiM parabhASArthaprakAzakAH?
Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
31 yUyaM zrESThadAyAn labdhuM yatadhvaM| anEna yUyaM mayA sarvvOttamamArgaM darzayitavyAH|
Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.

< 1 karinthinaH 12 >