< 1 karinthinaH 11 >

1 hE bhrAtaraH, yUyaM sarvvasmin kAryyE mAM smaratha mayA ca yAdRgupadiSTAstAdRgAcarathaitatkAraNAt mayA prazaMsanIyA AdhbE|
Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
2 tathApi mamaiSA vAnjchA yad yUyamidam avagatA bhavatha,
Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
3 Ekaikasya puruSasyOttamAggasvarUpaH khrISTaH, yOSitazcOttamAggasvarUpaH pumAn, khrISTasya cOttamAggasvarUpa IzvaraH|
Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
4 aparam AcchAditOttamAggEna yEna puMsA prArthanA kriyata IzvarIyavANI kathyatE vA tEna svIyOttamAggam avajnjAyatE|
Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
5 anAcchAditOttamAggayA yayA yOSitA ca prArthanA kriyata IzvarIyavANI kathyatE vA tayApi svIyOttamAggam avajnjAyatE yataH sA muNPitaziraHsadRzA|
Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
6 anAcchAditamastakA yA yOSit tasyAH ziraH muNPanIyamEva kintu yOSitaH kEzacchEdanaM zirOmuNPanaM vA yadi lajjAjanakaM bhavEt tarhi tayA svazira AcchAdyatAM|
Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
7 pumAn Izvarasya pratimUrttiH pratitEjaHsvarUpazca tasmAt tEna zirO nAcchAdanIyaM kintu sImantinI puMsaH pratibimbasvarUpA|
Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
8 yatO yOSAtaH pumAn nOdapAdi kintu puMsO yOSid udapAdi|
Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
9 adhikantu yOSitaH kRtE puMsaH sRSTi rna babhUva kintu puMsaH kRtE yOSitaH sRSTi rbabhUva|
Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
10 iti hEtO rdUtAnAm AdarAd yOSitA zirasyadhInatAsUcakam AvaraNaM dharttavyaM|
Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
11 tathApi prabhO rvidhinA pumAMsaM vinA yOSinna jAyatE yOSitanjca vinA pumAn na jAyatE|
Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
12 yatO yathA puMsO yOSid udapAdi tathA yOSitaH pumAn jAyatE, sarvvavastUni cEzvarAd utpadyantE|
Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
13 yuSmAbhirEvaitad vivicyatAM, anAvRtayA yOSitA prArthanaM kiM sudRzyaM bhavEt?
Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
14 puruSasya dIrghakEzatvaM tasya lajjAjanakaM, kintu yOSitO dIrghakEzatvaM tasyA gauravajanakaM
Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
15 yata AcchAdanAya tasyai kEzA dattA iti kiM yuSmAbhiH svabhAvatO na zikSyatE?
Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
16 atra yadi kazcid vivaditum icchEt tarhyasmAkam IzvarIyasamitInAnjca tAdRzI rIti rna vidyatE|
Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
17 yuSmAbhi rna bhadrAya kintu kutsitAya samAgamyatE tasmAd EtAni bhASamANEna mayA yUyaM na prazaMsanIyAH|
Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
18 prathamataH samitau samAgatAnAM yuSmAkaM madhyE bhEdAH santIti vArttA mayA zrUyatE tanmadhyE kinjcit satyaM manyatE ca|
Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
19 yatO hEtO ryuSmanmadhyE yE parIkSitAstE yat prakAzyantE tadarthaM bhEdai rbhavitavyamEva|
Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
20 Ekatra samAgatai ryuSmAbhiH prabhAvaM bhEjyaM bhujyata iti nahi;
Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
21 yatO bhOjanakAlE yuSmAkamEkaikEna svakIyaM bhakSyaM tUrNaM grasyatE tasmAd EkO janO bubhukSitastiSThati, anyazca paritRptO bhavati|
kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
22 bhOjanapAnArthaM yuSmAkaM kiM vEzmAni na santi? yuSmAbhi rvA kim Izvarasya samitiM tucchIkRtya dInA lOkA avajnjAyantE? ityanEna mayA kiM vaktavyaM? yUyaM kiM mayA prazaMsanIyAH? Etasmin yUyaM na prazaMsanIyAH|
Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
23 prabhutO ya upadEzO mayA labdhO yuSmAsu samarpitazca sa ESaH|
Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
24 parakarasamarpaNakSapAyAM prabhu ryIzuH pUpamAdAyEzvaraM dhanyaM vyAhRtya taM bhagktvA bhASitavAn yuSmAbhirEtad gRhyatAM bhujyatAnjca tad yuSmatkRtE bhagnaM mama zarIraM; mama smaraNArthaM yuSmAbhirEtat kriyatAM|
naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
25 punazca bhEjanAt paraM tathaiva kaMsam AdAya tEnOktaM kaMsO'yaM mama zONitEna sthApitO nUtananiyamaH; yativAraM yuSmAbhirEtat pIyatE tativAraM mama smaraNArthaM pIyatAM|
Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
26 yativAraM yuSmAbhirESa pUpO bhujyatE bhAjanEnAnEna pIyatE ca tativAraM prabhOrAgamanaM yAvat tasya mRtyuH prakAzyatE|
Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
27 aparanjca yaH kazcid ayOgyatvEna prabhOrimaM pUpam aznAti tasyAnEna bhAjanEna pivati ca sa prabhOH kAyarudhirayO rdaNPadAyI bhaviSyati|
Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
28 tasmAt mAnavEnAgra AtmAna parIkSya pazcAd ESa pUpO bhujyatAM kaMsEnAnEna ca pIyatAM|
Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
29 yEna cAnarhatvEna bhujyatE pIyatE ca prabhOH kAyam avimRzatA tEna daNPaprAptayE bhujyatE pIyatE ca|
Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
30 EtatkAraNAd yuSmAkaM bhUrizO lOkA durbbalA rOgiNazca santi bahavazca mahAnidrAM gatAH|
Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
31 asmAbhi ryadyAtmavicArO'kAriSyata tarhi daNPO nAlapsyata;
Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
32 kintu yadAsmAkaM vicArO bhavati tadA vayaM jagatO janaiH samaM yad daNPaM na labhAmahE tadarthaM prabhunA zAstiM bhuMjmahE|
Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33 hE mama bhrAtaraH, bhOjanArthaM militAnAM yuSmAkam EkEnEtarO'nugRhyatAM|
Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
34 yazca bubhukSitaH sa svagRhE bhugktAM| daNPaprAptayE yuSmAbhi rna samAgamyatAM| EtadbhinnaM yad AdESTavyaM tad yuSmatsamIpAgamanakAlE mayAdEkSyatE|
Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.

< 1 karinthinaH 11 >