< 32 >

1 Então aqueles três homens cessaram de responder a Jó, porque ele era justo em seus olhos.
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Porém se acendeu a ira de Eliú, filho de Baraquel, buzita, da família de Rão; contra Jó se acendeu sua ira, porque justificava mais a si mesmo que a Deus.
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Também sua ira se acendeu contra seus três amigos, porque não achavam o que responder, ainda que tinham condenado a Jó.
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 E Eliú tinha esperado a Jó naquela discussão, porque tinham mais idade que ele.
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 Porém quando Eliú viu que não havia resposta na boca daqueles três homens, sua ira se acendeu.
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 Por isso Eliú, filho de Baraquel, buzita, respondeu, dizendo: Eu sou jovem e vós sois idosos; por isso fiquei receoso e tive medo de vos declarar minha opinião.
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 Eu dizia: Os dias falem, e a multidão de anos ensine sabedoria.
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 Certamente há espírito no ser humano, e a inspiração do Todo-Poderoso os faz entendedores.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 Não são [somente] os grandes que são sábios, nem [somente] os velhos entendem o juízo.
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 Por isso eu digo: escutai-me; também eu declararei minha opinião.
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 Eis que eu aguardei vossas palavras, [e] dei ouvidos a vossas considerações, enquanto vós buscáveis argumentos.
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 Eu prestei atenção a vós, porém eis que ninguém há de vós que possa convencer a Jó, [nem] que responda a suas palavras.
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Portanto não digais: Encontramos a sabedoria; que Deus o derrote, [e] não o homem.
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 Jó não dirigiu suas palavras a mim, nem eu lhe responderei com vossos dizeres.
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 Estão pasmos, não respondem mais; faltam-lhes palavras.
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 Esperei, pois, porém [agora] não falam; porque já pararam, [e] não respondem mais.
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 Também eu responderei minha parte; também eu declararei minha opinião.
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 Porque estou cheio de palavras, e o espírito em meu ventre me obriga.
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 Eis que meu ventre é como o vinho que não tem abertura; e que está a ponto de arrebentar como odres novos.
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 Falarei, para que eu me alivie; abrirei meus lábios, e responderei.
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 Não farei eu acepção de pessoas, nem usarei de títulos lisonjeiros para com o homem.
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 Pois não sei lisonjear; [caso contrário], meu Criador logo me removeria.
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.

< 32 >