< Salmos 1 >

1 Bem-aventurado o homem que não anda no conselho dos maus, nem fica parado no caminho dos pecadores, nem se senta junto dos escarnecedores.
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Mas sim, que tem seu prazer na Lei do SENHOR; e medita em sua Lei de dia e de noite.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Porque ele será como uma árvore, plantada junto a ribeiros de águas, que dá fruto a seu [devido] tempo, e suas folhas não caem; e tudo quanto fizer prosperará.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 Os maus não são assim; mas são como a palha que o vento dispersa.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Por isso os maus não subsistirão no julgamento, nem os pecadores no ajuntamento dos justos.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 Porque o SENHOR conhece o caminho dos justos; porém o caminho dos maus perecerá.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Salmos 1 >