< Gálatas 1 >

1 Paulo apostolo (não da parte dos homens, nem por homem algum, mas por Jesus Christo, e por Deus Pae, que o resuscitou dos mortos)
Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
2 E todos os irmãos que estão comigo, ás egrejas da Galacia:
Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
3 Graça e paz de Deus Pae e de nosso Senhor Jesus Christo,
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
4 O qual se deu a si mesmo por nossos peccados, para nos livrar do presente seculo mau, segundo a vontade de Deus nosso Pae. (aiōn g165)
aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
5 Ao qual gloria para todo o sempre. Amen. (aiōn g165)
Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
6 Maravilho-me de que tão depressa passasseis d'aquelle que vos chamou á graça de Christo para outro evangelho.
Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
7 Que não é outro, mas ha alguns que vos inquietam e querem transtornar o evangelho de Christo.
Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
8 Mas, ainda que nós mesmos, ou um anjo do céu vos annuncie outro evangelho, além do que já vos tenho annunciado, seja anathema.
Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
9 Assim como já vol-o dissemos, agora de novo tambem vol-o digo. Se algum vos annunciar outro evangelho além do que já recebestes, seja anathema.
Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
10 Porque, persuado eu agora a homens ou a Deus? ou procuro comprazer a homens? se comprazera ainda aos homens, não seria servo de Christo.
Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
11 Mas faço-vos saber, irmãos, que o evangelho que por mim foi annunciado não é segundo os homens.
Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
12 Porque não o recebi, nem aprendi de homem algum, mas pela revelação de Jesus Christo.
Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
13 Porque já ouvistes qual foi antigamente a minha conducta no judaismo, que sobremaneira perseguia a egreja de Deus e a assolava.
Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
14 E como na minha nação excedia em judaismo a muitos da minha edade, sendo extremamente zeloso das tradições de meus paes.
Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
15 Mas, quando approuve a Deus, que desde o ventre de minha mãe me separou, e me chamou pela sua graça,
Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
16 Revelar seu Filho em mim, para que o prégasse entre os gentios, não consultei a carne nem o sangue,
kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
17 Nem tornei a Jerusalem, a ter com os que já antes de mim eram apostolos, mas parti para a Arabia, e voltei outra vez a Damasco.
na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
18 Depois, passados tres annos, fui a Jerusalem para ver a Pedro, e fiquei com elle quinze dias.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
19 E não vi a nenhum outro dos apostolos, senão a Thiago, irmão do Senhor.
Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
20 Ora, ácerca das coisas que vos escrevo, eis que diante de Deus testifico que não minto.
Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
21 Depois fui para as partes da Syria e da Cilicia.
Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
22 E não era conhecido de vista das egrejas da Judea, que estavam em Christo;
Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
23 Mas sómente tinham ouvido dizer: Aquelle que d'antes nos perseguia annuncia agora a fé que d'antes destruia.
lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
24 E glorificavam a Deus a respeito de mim.
Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.

< Gálatas 1 >